Dar es Salaam. Wasanii wanne wa filamu nchini wameondoka nchini
usiku wa kuamkia jana kwenda Uturuki, ambako watajifunza utamaduni wa
nchi hiyo pamoja na kukutana na wasanii wakubwa wa filamu wa nchi
hiyo.Wasanii walioondoka nchini ni pamoja na Amri Athumani ‘Mzee
Majuto’, Vincent Kigosi ‘Ray’, Irine Uwoya na Jacob Steven ‘JB’.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, JB alisema ziara
hiyo ya wiki moja itawapa fursa ya kushirikiana na kubadilishana uzoefu
wa kikazi na wenzao wa Uturuki.
“Tukiwa Uturuki tutakutana na wataalamu wa mambo
ya filamu, hivyo tutajifunza mambo mapya, lakini pia tutabadilishana
uzoefu na wenzetu wa Ururuki.
“Ni matumaini yangu kile tutakachojifunza Uturuki
kitatusaidia kutengeneza filamu bora zaidi tutakaporudi nchini na
kuifanya Tanzania kuwika kimataifa,” alisema JB.
Naye meneja mkuu wa Princess Cassino, Ali Aiden
alisema: “Tumeamua kuwafadhili wasanii hawa kama njia mwafaka ya
kuonyesha kwamba tunaunga mkono jitihada zao za kukuza tasnia ya filamu
nchini.”
Balozi wa Uturuki nchini, Ali Dovutoglu alisema:
“Ziara ya wasanii hao ni matunda ya ushirikiano mzuri kati ya Uturuk na
Tanzania, ambayo tangu nimekuja hapa nimebaini ni nchi yenye utulivu wa
hali ya juu.”
Post a Comment