Ben Pol ameiambia Bongo5 kuwa ni kawaida yake kila mwezi wa nane au wa tisa kuachia wimbo wenye mahadhi ya R&B ambayo mashabiki wake wengi wamemzoea akiimba hivyo.
“Hata ukiangalia mwaka jana ilikuwa ‘Wa Ubani’, mwaka juzi ilikuwa ‘Pete’, mwaka wa nyuma yake ilikuwa ‘Numbe 1 Fan’, mwaka wa nyuma yake ulikuwa ‘Nikikupata’,” amesema Ben Pol.
Akizungumzia sababu za kufanya wimbo wa DX, Ben Pol amesema producer huyo wa Arusha ana beats nyingi za R&B kwenye maktaba yake hivyo ilikuwa rahisi wawili hao kupata kitu cha kurekodi.
‘Twaendana’ unapatikana kwenye mtandao wa mkito.com.
Post a Comment