Wateja wakinunua nyama ya ng’ombe ndani ya machinjio ya Vingunguti, Dar es Salaam. Rafael Lubava
Dar es Salaam. Ukiwa unakaribia katika eneo la
machinjio lililopo Vingunguti jijini hapa kabla ya kuingia ndani salamu
ya kwanza utakayopokelewa nayo ni “Karibu mteja fungu moja ni Sh
1,000 tu…dada karibu uboreshe ndoa…kaka karibu uboreshe ndoa,”hizo ni
sauti za vijana waliopanga bidhaa zao kwenye meza pembezoni mwa Barabara
ya Vingunguti, nje ya banda la kuchinjia mifugo.
Lakini licha ya salamu yao nzuri ya ukarimu
iliyojaa mbwembwe nyingi, huenda ukashindwa kuitikia kutokana na harufu
mbaya na hewa nzito iliyozingira anga la hapa. Unaweza ukawa unazuia ile
hewa isiingie ndani ya kinywa chako. Ukaziba mdomo na pua kidogo
kuruhusu hewa kiasi kupita. Ila kwa wenyeji wa hapa inaonekana hilo siyo
tatizo kwao, wanaendelea kupiga mzigo. Wengine wanapata vifungua kinywa
bila wasiwasi.
Salamu hiyo ndiyo kivuto kwa wateja. Hii ndiyo
chachu kwao ili wasogee karibu kupata huduma hiyo, hasa wakinamama. Na
ndivyo na mimi nilivyovutiwa na kusogea karibu kutaka kufahamu undani wa
bidhaa hizo.
Ilipofika saa moja kasoro asubuhi. Hapa kila mmoja anajitahidi kuhakikisha anamvutia mteja kwa upande wake.
Lengo ikiwa ni mteja hapiti bila kununua
chochote. Japo kuna wakati mwingine hali huwa tofauti kwani si kila
anayepita barabarani hapo huwa na lengo la kununua nyama, wengine ni
wapita njia tu. Ndiyo biashara.
Kama mmoja wa wapitanjia ambaye niligeuka kuwa
mteja nilisogea karibu. Nilitaka kufahamu undani wa bidhaa hizi. Shauku
hiyo haikuja hivihivi bali ni kutokana na maneno ambayo yanasemwa
mitaani.
Ukipita mitaani utasikia watu wakisema mambo mengi
juu ya machinjioni. Baadhi husema kuwa kuna watu kazi yao ni kuokota
baadhi ya masalia ya nyama za ng’ombe. Wakishaokota mabaki hayo huyauza
kwa bei ndogo ukilinganisha na ile ya buchani.
Kwa sasa kilo moja nyama huuzwa kwa Sh5,000 hadi
Sh 6,000. Bei ya hawa jamaa ni tofauti kidogo. Unafuu wa bei yao
hautokani na yale madai kuwa wao huokota masalia na kwenda kuuzia watu
iwe nje ya machinjio ua sehemu nyingine huko mitaani. Wanasema sababu ni
kuwa wao wapo kiwandani.
Maneno hayo ananiambia kijana mmoja anayeuza nyama
nje ya machinjio hayo aliyejitambulisha kwa jina la Daniel Lucas. Ni
mmoja kati ya vijana wachacharikaji kweli ambao wamepanga mstari wa meza
zenye mafungu ya nyama tofauti.
Juu ya meza kila moja kuna mafungu kama kumi hivi
ya nyama. Wengine wameweka nyama za utumbo, wengine steki na wengine
maini. Wakati huo pilika za kuwahudumia wateja zinaendelea. Vijana
wengine wanaonekana kuwahudumia huku wengine wakiendelea kukata nyama na
kuzipanga mezani.
Chini ya kila meza kuna ndoo yenye maji ndani yake
kuna nyama. Ikabidi nihoji kwanini wanafanya hivyo, “Huwa tunasafisha
nyama kabla ya kuzipanga mezani. Wakati mwingine tunanyunyizia hayo maji
kwenye nyama ili zisiharibike kama siku hiyo hakuna wateja na nyama
ikachelewa kuisha,” anasema Lucas. Baada ya kusonga karibu ili kujionea
nyama hizo na maji. Mazingira ya pale hayakuwa rafiki sana kwa maana ya
usalama wa afya ya mlaji.
Majibu hayo bado si ya kuridhika nayo kutokana na
ile hali ya usafi wa eneo lile. Ile hali ya kumwaga maji inafanya chini
kuwe na matope, inzi lakini wao hawaonekani kujalii ile hali hata
kidogo. Pia mimi pia napiga moyo konde naendelea kuka nao kwa muda wa
dakika kadhaa.
Wateja wanakuja na kuondoka. Kuna wanaokuja na kuuliza. Wengine
wanauliza bei na kununua. Kwa wanunuaji, akichukua fungu moja au mawili
ya nyama anawekewa kwenye mfuko mweusi na kuondoka.
Lucas anasema kwa malipo ya kila fungu la nyama
ya utumbo ni Sh1,000. Hapa hakuna kupunguziwa. Hakuna kipimo. Kipimo
wanakijua wao wenyewe. Ila kwa wanunuaji kipimo ni macho yao. Licha ya
kuwa macho yanaweza kudanganya. Mizani ndiyo ingekuwa wakili pekee na
msema kweli na mtenda haki hapa, lakini kwa wafanyabiashara wa hapa hali
siyo hivyo.
Kwa upande wa nyama ya steki kijana huyo anasema
kuwa fungu moja ni Sh2,000. Mfumo ule ule, hakuna mizani. Mafungu
yamewekwa kazi ni kwako mteja kuchagua fungu ambalo unapendezwa nalo.
Namuuliza huyu kijana kwa nini hawapimi nyama kwa kutumia mizani.
“Unajua dada haya mafungu tunayoweka hapa bei
yake ni sawa na bure…Sisi ni kama tunagawa tu nyama kwa wateja wetu. Wee
nenda ukapime hilo fungu moja ulilochukua halafu ukirudi utatuambia.
Kama ingekuwa tunapunja tusingekuwa tunapata wateja…kwanza mashine ni
mizingo tu hapa tutaweka wapi mazingira yenyewe si unayaona,”alijitetea
Lucas kwa ujasiri.
Niliposogea mezani vilivyokuwa vimemwagwa vipande
vya steki hali ilikuwa ilele. Kilichonifurahisha kwa upande wa steki.
Ukifika hawa vijana wanahakikisha wamekupa mfuko wa plastiki. Huo mfuko
unavaa mkononi kabla ya kuanza kuchagua kipande cha nyama. Tofauti na
kwenye utumbo. Hapa usafi kidogo unazingatiwa.
Kwenye maini nako ni kama kule kwa utumbo. Unachagua kipande na kulipia Sh2,000 kisha unaondoka.
Wanunuaji wengine ndiyo wale wanaoonekana pembeni
wakiwa katika pilikapilika za kutengeneza mishikaki na kuchemsha supu.
Mishikaki na supu huenda sambamba na mihogo ambayo inakaangwa na
kinamama wa hapa. Kama ni mgeni wa hili eneo kwa mara ya kwanza lazima
utajiuliza maswali mengi kabla ya kuchukua uamuzi wa kukaa na kutia kitu
chochote kinywani.
Mazingira ambayo vitu hivi vinatengenezwa siyo
mazuri kwa afya hata kidogo. Kwanza ile hali ya unyevunyevu, matope na
inzi wanaozunguka kila kona ya eneo hilo la machinjio. Asili tu ya eneo
hilo inatosha kulifanya kuwe na harufu ambayo inachangia kuwapo kwa inzi
wengi. Baadhi ya sehemu zina vinyesi vya wanyama ambao wameletwa kwa
ajili ya kuchinjwa.
Bado eneo hilo hilo watu wanatumia kufanya biashara ya chakula. Pia watu wameketi wanakula na kunywa.
Wafanyabishara hao wengine wamegawanyika katika
makundi matatu. Wakaanga mihogo, wauza supu pamoja na chapati na
maandazi, pombe za kisasa na kienyeji, wauza nyanya vitunguu na
mbogamboga nyingine na waendesha bodaboda. Hawa wapo sambamba na wateja
wao pia.
Wateja wamekaa katika makundi. Kwenye mabenchi.
Kuna wanaokula mihogo, kuna wa chapati na supu. Pombe za kienyeji ile ya
kule uchagani mbege.Walionifurahisha ni wale waliokuwa wanakunywa bia.
Walikuwa wamekaa kwenye benchi pia. Kila kundi la watu watatu au wanne
walikuwa na kreti lao la bia, wamekaa kwenye kona.
Dar es Salaam. Ukiwa unakaribia katika eneo la
machinjio lililopo Vingunguti jijini hapa kabla ya kuingia ndani salamu
ya kwanza utakayopokelewa nayo ni “Karibu mteja fungu moja ni Sh
1,000 tu…dada karibu uboreshe ndoa…kaka karibu uboreshe ndoa,”hizo ni
sauti za vijana waliopanga bidhaa zao kwenye meza pembezoni mwa Barabara
ya Vingunguti, nje ya banda la kuchinjia mifugo.
Lakini licha ya salamu yao nzuri ya ukarimu
iliyojaa mbwembwe nyingi, huenda ukashindwa kuitikia kutokana na harufu
mbaya na hewa nzito iliyozingira anga la hapa. Unaweza ukawa unazuia ile
hewa isiingie ndani ya kinywa chako. Ukaziba mdomo na pua kidogo
kuruhusu hewa kiasi kupita. Ila kwa wenyeji wa hapa inaonekana hilo siyo
tatizo kwao, wanaendelea kupiga mzigo. Wengine wanapata vifungua kinywa
bila wasiwasi.
Salamu hiyo ndiyo kivuto kwa wateja. Hii ndiyo
chachu kwao ili wasogee karibu kupata huduma hiyo, hasa wakinamama. Na
ndivyo na mimi nilivyovutiwa na kusogea karibu kutaka kufahamu undani wa
bidhaa hizo.
Ilipofika saa moja kasoro asubuhi. Hapa kila mmoja anajitahidi kuhakikisha anamvutia mteja kwa upande wake.
Lengo ikiwa ni mteja hapiti bila kununua
chochote. Japo kuna wakati mwingine hali huwa tofauti kwani si kila
anayepita barabarani hapo huwa na lengo la kununua nyama, wengine ni
wapita njia tu. Ndiyo biashara.
Kama mmoja wa wapitanjia ambaye niligeuka kuwa
mteja nilisogea karibu. Nilitaka kufahamu undani wa bidhaa hizi. Shauku
hiyo haikuja hivihivi bali ni kutokana na maneno ambayo yanasemwa
mitaani.
Ukipita mitaani utasikia watu wakisema mambo mengi
juu ya machinjioni. Baadhi husema kuwa kuna watu kazi yao ni kuokota
baadhi ya masalia ya nyama za ng’ombe. Wakishaokota mabaki hayo huyauza
kwa bei ndogo ukilinganisha na ile ya buchani.
Kwa sasa kilo moja nyama huuzwa kwa Sh5,000 hadi
Sh 6,000. Bei ya hawa jamaa ni tofauti kidogo. Unafuu wa bei yao
hautokani na yale madai kuwa wao huokota masalia na kwenda kuuzia watu
iwe nje ya machinjio ua sehemu nyingine huko mitaani. Wanasema sababu ni
kuwa wao wapo kiwandani.
Maneno hayo ananiambia kijana mmoja anayeuza nyama
nje ya machinjio hayo aliyejitambulisha kwa jina la Daniel Lucas. Ni
mmoja kati ya vijana wachacharikaji kweli ambao wamepanga mstari wa meza
zenye mafungu ya nyama tofauti.
Juu ya meza kila moja kuna mafungu kama kumi hivi
ya nyama. Wengine wameweka nyama za utumbo, wengine steki na wengine
maini. Wakati huo pilika za kuwahudumia wateja zinaendelea. Vijana
wengine wanaonekana kuwahudumia huku wengine wakiendelea kukata nyama na
kuzipanga mezani.
Chini ya kila meza kuna ndoo yenye maji ndani yake
kuna nyama. Ikabidi nihoji kwanini wanafanya hivyo, “Huwa tunasafisha
nyama kabla ya kuzipanga mezani. Wakati mwingine tunanyunyizia hayo maji
kwenye nyama ili zisiharibike kama siku hiyo hakuna wateja na nyama
ikachelewa kuisha,” anasema Lucas. Baada ya kusonga karibu ili kujionea
nyama hizo na maji. Mazingira ya pale hayakuwa rafiki sana kwa maana ya
usalama wa afya ya mlaji.
Majibu hayo bado si ya kuridhika nayo kutokana na
ile hali ya usafi wa eneo lile. Ile hali ya kumwaga maji inafanya chini
kuwe na matope, inzi lakini wao hawaonekani kujalii ile hali hata
kidogo. Pia mimi pia napiga moyo konde naendelea kuka nao kwa muda wa
dakika kadhaa.
Post a Comment