0
Dar es Salaam. Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij na wachezaji wake wameahidi ushindi wa kishindo kesho dhidi ya  Msumbiji huku wakiwataka Watanzania kufika kwa wingi uwanjani kutoa sapoti.
Stars na  Msumbiji zitashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa kusaka kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika 2015, Morocco.
Kocha Nooij alisema wachezaji wake wote wako fiti kwa ajili ya mchezo huo na anatambua ugumu wa mechi hiyo, lakini amewataka watanzania kutoa sapoti kwani timu hiyo ni ya wote.
“Itakuwa moja ya mechi ngumu, lakini wachezaji wangu wote wako tayari kwa ajili ya mchezo huo, naijua Msumbiji kwani nimewahi kufundisha huko hivyo nafahamu mbinu zao na nimeshawaandaa wachezaji wangu na kuwapa mbinu jinsi ya kuwadhibiti.”
Naye nahodha wa Stars,  Nadir Haroub ‘Canavaro’, alisema wamejiandaa vizuri na wamerekebisha makosa yote yaliyojitokeza katika michezo iliyopita hasa safu ya ulinzi na kudai  watahakikisha wanalipiza kisasi na kuhakikisha wanashinda mchezo huo.
“Bado nakumbuka kipigo tulichopata kutoka kwa Msumbiji mwaka 2007 wakati Nooj akiwa kocha wa timu hiyo na sasa ni muda wa kulipa kisasi kwa timu hiyo nikiwa chini ya kocha huyo na nitahakikisha  najituma kwa faida ya Watanzania na yangu binafsi na nitahamasisha wenzangu kujituma zaidi ili tuweze kushinda mchezo huo,” alisema Canavaro.

Post a Comment

 
Top