0
Dar es Salaam. Timu ya taifa ya soka ya vijana chini ya miaka 17, Ngorongoro Heroes imeshindwa kutamba mbele ya wenzao wa Afrika Kusini, baada ya kulazimishwa suluhu nyumbani.
Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, ulikuwa na nafasi kadhaa za kufunga kwa kila timu lakini zilitumiwa vibaya.
Mchezo huo ni wa kuwania nafasi ya kufuzu kwa fainali za Afrika kwa vijana wa umri huo zitakazofanyika Niger, ambapo mchezo wa marudiano utapigwa nchini Afrika Kusini baada ya wiki mbili.
Serengeti Boys walianza vizuri katika kipindi cha kwanza, lakini nafasi zilikuwa chache na nzuri kupitia kwa Athanas Mdamu, ambaye alionekana huenda angeweza kuitoa Tanzania kimasomaso.
Licha ya kupata nafasi kadhaa katika kipindi cha kwanza, hali hiyo haikusaidia hata katika kipindi cha pili, wakati Khanyiso Mayo wa Afrika Kusini akionekana kuwa msumbufu, lakini uimara wa kipa wa Serengeti, Metacha Mnata alifanya kazi ya ziada.

Post a Comment

 
Top