0
Mkinga. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa ameishangaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga kuweka ushuru wa mkaa kama eneo la ukusanyaji wa mapato ya ndani na kutaka biashara hiyo ikome kwa sababu madhara yake ni makubwa katika uharibifu wa mazingira.
Alisema hayo alipokutana na wakuu wa idara pamoja na madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo.
Gallawa aliwataka wakuu wa idara pamoja na wataalamu wa halmashauri hiyo kutumia elimu zao kubuni njia za kuwaongezea vipato wananchi ili hatimaye wawe na uwezo wakuchangia shughuli za maendeleo. “Haiwezekani, halmashauri iweke katika mipango yake ushuru wa mkaa na kuni kama sehemu ya mapato, yaani inabariki uharibifu wa mazingira kwa makusanyo ya siku chache yatakayosababisha jangwa la kudumu,” alihoji Gallawa.

Post a Comment

 
Top