Mashabiki katika mji mkuu wa Costa Rica, San Jose,
walikusanyika katika eneo la Fuente de la Hispanidad, eneo ambalo
hutumika kwa ajili ya sherehe za kitamaduni, wakiwa na bendera za taifa
lao, nywele bandia na jezi zao wakiishangilia timu yao kwa ushindi wa
mikwaju ya penalti.
‘”Taifa limeanguka. Kunaweza kuwa na tetemeko la
ardhi,” alinukuliwa akisema mhudumu wa mgahawa, Teo Prestinary (43),
katika fukwe za Nosara, ambapo kulikuwa na watu wengi wakishangilia kwa
kuimba wimbo wa ‘Vamos Ticos’ (Go, Costa Ricans).
Maria Mendoza, mwenye miaka 33, alishuhudia
shamrashamra hizo kupitia runinga akiwa mjini Santa Ana, alisema: “Ni
furaha, furaha, furaha iliyopitiliza.”
Costa Rica ilifikia hatua ya kuitoa Ugiriki baada
ya kuzichapa Uruguay na Italia na kulazimisha sare na England, wakati
ilitabiriwa kuwa ndiyo timu dhaifu katika kundi lao.
Na walishinda kwa mikwaju ya penalti 5-3 baada ya
mchezo wao kumalizika kwa sare ya bao 1-1 katika dakika 120. Na sasa
Costa Rica wanasema kufika mbali zaidi.
“Siku zote huwa tuna matumaini,” alisema Luis
Diego Escorriola, shabiki mwenye miaka 42, ambaye alikuwa akifuatilia
mchezo huo kwenye runinga kabla ya kujiunga na wenzake mitaani
kushangilia.
Post a Comment