Dar es Salaam.Watumiaji wa huduma za kibenki
wametakiwa kujiepusha na wimbi kubwa la utapeli kwa njia ya mtandao
linaonekana kushika kasi siku za hivi karibuni.
Wametakiwa pia kutokubali kutoa taarifa zao kwa watu wasiowafahamu kutokana na wengi wao kutumia fursa hiyo kufanya uhalifu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk Charles Kimei kuhusu huduma ya kutuma na
kutoa pesa kupitia simu za mkononi (Simbanking) na changamoto ya uhalifu
kwa njia ya mtandao aliwataka wateja wa benki kutunza taarifa za
akaunti zao ikiwemo kadi na namba za siri.
“Wote tunafahamu kuwa kumeibuka matapeli kwenye
mitandao ya kijamii wanaojaribu kuwalaghai wateja wetu kwa kuwaomba
taarifa za akaunti zao ili kufanya uhalifu,”alisema na kuongeza:
“Tunawaomba wateja wetu kuwa makini na matapeli
wanaopiga simu kujitambulisha kuwa ni wafanyakazi wa CRDB wakiwataka
watoe maelezo ya akaunti zao ikiwemo namba za siri, vilevile niwasihi
wasitumie mwaka wa kuzaliwa kama namba ya siri na kuepuka kutunza namba
hizo kwenye simu au anuani zao za mtandao.”
Hata hivyo, Dk Kimei aliwaondoa hofu wateja wa
benki hiyo wanaotumia huduma ya Simbanking akisema kuwa imehakikiwa na
imepitia viwango vyote vya usalama.
Post a Comment