0
Arusha. Baadhi ya mashabiki, wadau na wapenzi wa soka jijini Arusha wamelalamikia hali ya uchafu wa vyoo vilivyopo ndani ya uwanja wa michezo wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid wakisema vyoo hivyo mbali na kutoa harufu, lakini vinaweza kusababisha madhara kiafya kwa binadamu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi katika siku ya wauguzi duniani iliyoadhimishwa kitaifa mkoani Arusha, baadhi ya wakazi wa jiji hilo, walisema ni aibu kwa wamiliki wa uwanja huo ambao ni Chama Cha Mapinduzi kushindwa kufanya usafi wa vyoo hivyo.
“Hii ni aibu kubwa kwa wamiliki wa uwanja huu, ambao ni chama tawala, vyoo vinatoa harufu nzito, ni hatari kwa afya,” walisema kwa nyakati tofauti
Diwani wa Kata ya Moshono, Paul Mathysen, aliliambia gazeti hili kuwa alipata fursa ya kufika katika vyoo hivyo juzi wakati wa sherehe hizo lakini kutokana na hali ya uchafu aliyoikuta alishindwa kupata huduma.
Baadhi ya vibarua wanaofanya usafi ndani ya uwanja huo walipohojiwa hawakutaka kuzungumzia suala hilo, lakini alipotafutwa Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM mkoani Arusha, Hilal Sood, naye alikwepa kutoa taarifa kwa gazeti  hili pamoja na kutafutwa mara kwa mara

Post a Comment

 
Top