0
Tatizo la ufungaji limeendelea kuwaandama washambuliaji wa Tanzania katika Ligi Kuu hadi sasa ni Haruna Chanongo pekee anayecheza katika kikosi timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), aliyefunga mabao matatu katika mzunguko huu wa nne wa ligi hiyo.
Katika orodha ya wafungaji hadi sasa mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi na Simba, Amis Tambwe anaongoza  akiwa amezifumania nyavu mara sita katika mechi tatu alizoshuka di
mbani.
Mrundi huyo anafuatiwa kwa mbali na Chanongo pamoja na washambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu na Jerryson Tegete ambao kila mmoja amefunga mabao matatu hadi sasa.
Hata hivyo,Tegete kwa muda mrefu sasa hayumo katika kikosi cha Stars kinachonolewa na kocha Kim Poulsen.
Mshambuliaji mwingine wa Stars aliyeingia katika orodha ya wafumania nyavu ni John
Bocco ambaye amefunga bao moja pekee.
Bocco anayetajwa  kama mmoja wa washambuliaji bora wa Tanzania msimu huu ameshindwa kuonyesha makali kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara. Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopia Kipre Tchetche wa  Azam FC  amefumania nyavu mara mbili.

Post a Comment

 
Top