Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Simba,
Betram Mombeki amesema atahakikisha anaiongoza timu hiyo kutwaa ubingwa
wa Lligi Kkuu msimu huu.
Mombeki ameendelea kuyafurahia maisha ndani ya klabu hiyo na kuonekana kuridhishwa na ufundi wa kocha wao, Abdallah Kibadeni.
A amesema hana wasiwasi na uchanga wa kikosi hicho na anaamaini bado Simba ina uwezo wa kunyakua ubingwa.
Akizungumza mara baada ya mchezo wao wa kirafiki
wa kimataifa dhidi ya SC Villa ya Uganda ambapo Simba iliibuka na
ushindi wa mabao 4-1, huku Mombeki akifunga magoli mawili peke yake
alisema chipukizi wa Simba wataiwashangaza mashabiki kwa soka safi
watakalokuwa wakicheza.
“Sina shaka na kikosi chetu, ni kweli bado
kichanga na wachezaji kama mnavyowaona wengi ni wageni, lakini hii
haimaanishi tutashindwa kurudisha heshima ya Simba ya kutwaa ubingwa,
nategemea ushirikiano wa wachezaji wenzangu na juhudi ziutatuweka katika
nafasi nzuri zaidi,” alisema mshambuliaji huyo.
Katika hatua nyingine, Mombeki amewatahadharisha
vinara wa ufungaji katika ligi hiyo na kudai lengo lake ni kuwa mfungaji
bora wa ligi.
Simba inajiandaa na mchezo mwingine wa kirafiki
utakaopigwa kesho kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya Three Pillars ya
Nigeria.Subhead andika hapa , andika hapa,andika hapa Subhead andika
hapa andika, andika hapa, subhead andika hapa, andika hapa,
Post a Comment