0
Morogoro. Baadhi ya wananchi wa mkoani Morogoro wametoa maoni yao kuhusiana na rasimu ya Katiba Mpya ambayo ilizinduliwa Juni 3 mwaka huu jijini Dar es Salaam na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Mohamed Gharib Bilal.
Wananchi hao ni pamoja na wanaharakati, wasomi wa vyuo vikuu pamoja na watendaji wa mamlaka na idara mbalimbali za Serikali wengi wao walionyeshwa kuridhishwa na rasimu hiyo.
Akizungumzia rasimu hiyo, Robert Selasela ambaye ni msomi wa Chuo Kikuu Mzumbe alisema endapo rasimu hiyo itapitishwa kipengere cha Spika na Naibu Spika kutotoka kwenye vyama kutaweza kusaidia kuondoa malalamiko na malumbano yanayotokea bungeni.
Kwa upande wake Richard Kabate ambaye ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa alisema kuwa kuanzishwa kwa Mahakama ya Juu kutaweza kupanua wigo wa utoaji na upatikanaji wa haki kwani wananchi watakuwa na uwezo wa kukata rufaa katika mahakama tatu tofauti.
Naye Amani Mwaipaja ambaye ni mwanasheria wa kujitegemea na mwanaharakati wa haki za binadamu alisema kuwa kuwekwa kwa kiwango cha elimu kwa Spika, Naibu Spika na wagombea wa nafasi nyingine kutasaidia kuondokana na tatizo la kuwa na viongozi wasio wasomi ambao wamekuwa wakishindwa kuchambua mambo muhimu yanayohusu nchi.
kwamba kutasaidia kuondokana na kero za Muungano ambazo zimekuwa zikilalamikiwa kwa kipindi kirefu bila ufumbuzi.

Post a Comment

 
Top