0


 
 
Na Mwandishi Wetu  (email the author)


Dar es Salaam. Benki ya Exim Tanzania imeendelea kujiimarisha kwa Sekta ya Benki baada ya kutajwa katika utafiti uliofanywa na Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Hesabu ya KPMG, kuwa miongoni mwa benki zinazowajali wateja nchini.
Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa na KMPG kwa Sekta ya benki kwenye nchi 14 barani Afrika, ulihusisha masuala mbalimbali ya huduma kwa wateja.
Utafiti huo ulifanyika kati ya Juni na Desemba mwaka jana, Benki ya Exim iliongoza kwa kujali wateja wake nchini ikifuatiwa za Benki ya Barclays na Akiba Commercial (ACB).
“Benki ya Exim imeweza kupata alama 75.2 kwa jumla kwenye suala la kumjali mteja, ikifuatiwa na Barclays alama 75 na Akiba Commercial Bank (ACB) alama 74.9,” ripoti hiyo inasema.
Akizungumzia utafiti huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim Tanzania, Anthony Grant alisema matokeo hayo ni changamoto kwa benki yake na kwamba, wataongeza juhudi ili kupata mafanikio zaidi miaka ijayo. “Huu ni mwaka mzuri kihistoria kwa benki yetu. Matokeo haya ya utafiti yamekuja muda mfupi baada ya benki kuteuliwa katika Tuzo ya Benki Bora barani Afrika mwaka huu,” alisema.

Post a Comment

 
Top