0
Katika Uwanja wa wazi mji wa E'el Ali iliyo katika mkoa wa Hiraan katikati mwa Ardhi ya Somalia jana ilifanyika hukumu ya Haddi ya Jaldi ambayo ilitekelezwa kwa mwanaume anaejulikana kwa jina la Bashir Ibrahim Abdullahi aliyembaka mwanamke aliyekuwa na mtoto mchanga.


Mwanaume huyo aliyeshtakiwa na Mlalamikaji ambae ndie aliyetendewa unyama huo amekiri mbele ya Mahakama kuwa alifanya kitendo hicho huko akiwa na akili yake timamu wakati akitenda kosa hilo,baada ya kusikiliza kesi hiyo Mahakama ilitoa na kutangaza hukumu.



Bashir alihukumiwa kulipa Mahari ya Mwanamama huyo,na kuhamishwa kutoka katika mji huo kwa muda wa mwaka mmoja,kuchapwa viboko 100 mbele ya kadamnasi waliohudhuria kushuhudia hukumu hiyo ikitekelezwa.


Katika Mikoa ya Kiislaam nchini Somalia yalio chini ya Utawala wa Mujahidina wanawake wa Kiislaam wamepata Heshima na Izza huko wakiwa huru kwenda kokote watakao bila kubughudhiwa lakini maeneo yanayoshikiliwa na Maadui wanawake wa Kiislaam hupata madhila na kuchezewa heshima na karama zao.

Post a Comment

 
Top