Jana usiku watu waliokuwa wamejihami na silaha mbalimbali wamewapiga
risasi na kuwaua papo hapo baadhi ya Maaskari wa Serikali ya FG
waliokuwa wakiwasumbua wananchi na kuchukua pesa zao kwa nguvu ndani ya
mji wa Afgooye.
Maaskari
hao waliouwa walikuwa wawili waliokuwa maarufu katika soko la mji wa
Afgooye na ghafla walikutana na wanaume aliokuwa na silaha na kisha
kuanza kuwamiminia risasi hadi wanakata roho kama walivyoarifu mashuhuda
waliokuwepo katika tukio hilo.
Milio
ya risasi waliomiminiwa yalisikika baadhi ya maeneo mengi ya mji wa
Afgooye huko taarifa zikiongeza kuwa miili ya wanamgambo hao waliouwa
yaliondolewa baadae ktika eneo waliopigiwa risasi.
Wakaazi
wa mji wa Afgooye asubuhi ya leo wameanza kuepukana na shari ya
wanamgambo hao waliokuwa kero kwa waislaam wanaoishi katika mji huo.
Post a Comment