0
Jana usiku watu waliokuwa wamejihami na silaha mbalimbali wamewapiga risasi na kuwaua papo hapo baadhi ya Maaskari wa Serikali ya FG waliokuwa wakiwasumbua wananchi na kuchukua pesa zao kwa nguvu ndani ya mji wa Afgooye.


Maaskari hao waliouwa walikuwa wawili waliokuwa maarufu katika soko la mji wa Afgooye na ghafla walikutana na wanaume aliokuwa na silaha na kisha kuanza kuwamiminia risasi hadi wanakata roho kama walivyoarifu mashuhuda waliokuwepo katika tukio hilo.



Milio ya risasi waliomiminiwa yalisikika baadhi ya maeneo mengi ya mji wa Afgooye huko taarifa zikiongeza kuwa miili ya wanamgambo hao waliouwa yaliondolewa baadae ktika eneo waliopigiwa risasi.


Wakaazi wa mji wa Afgooye asubuhi ya leo wameanza kuepukana na shari ya wanamgambo hao waliokuwa kero kwa waislaam wanaoishi katika mji huo.

Post a Comment

 
Top