Habari iliyotufikia kutoka katika miji ya Kaskazini Mashariki nchini
Kenya khususan katikati mwa maeneo ya mji wa Madera na Al Arabia
zinaaifu kuwa watu waliokuwa na silaha wamefanya shambulio na
kusimamisha Basi waliokuwemo Abiria au wasafiri.
Habari
zaidi zinaeleza kuwa watu hao waliofanya shambulio hilo baada ya
kusimamisha basi hilo walianza kufanya upekuzi ndani ya Basi na kuanza
kuwateremsha Abiria na kisha kuondoka nae Afisa mmoja wa Serikali katika
County ya Mandera na baadhi ya vijiji vilio chini ya County hiyo.
Watu
hao waliotekeleza shambulio hilo inaarifiwa waliondoka na Afisa huyo na
kuiruhusu Gari hilo na Abiria wake waliokuwemo kwenye Basi hilo,mpaka
sasa haijajulikana walikoenda nae Afisa huyo wa Serikali ya Kenya na
hakuna maelezo yeyote kwa kikosi gani kilichotekeleza shambulio hilo.
Vyombo
vya habari nchini Kenya vimewanukuu baadhi ya viongozi upande wa
usalama wamethibitisha kutokea shambulio hilo iliyomteka kiongozi wa
Serikali ya Utawala wa mji wa Mandera iliyo sehemu ya Ardhi inayokaliwa
kwa Mabavu.
Post a Comment