0
Kuna maelezo zaidi yaliopatikana kuhusiana na shambulio lililofanyika jana usiku katika mji wa Bosaso makao makuu ya mkoa wa Kaskazini Mashariki mwa Somalia.



Mashambulio hayo yaliokuwa ya kufuatana yalilenga eneo ambalo ulinzi wake uliimarishwa vilivyo,shambulio la kwanza iliyofanyika nje ya lango kuu la Ikulu ya Rais waliuliwa Maaskari wawili wa Utawala wa Puntland.



Shambulio lingine lililofanyika katika mtaa wa New Bosaso imesababisha kujeruhiwa vibaya mkuu wa Wilaya wa Armo katika utawala wa "Puntland".


Duru za kuaminika zilieleza kuwa Mohamed Shire ambae alikuwa mkuu wa Wilaya wa Armo amepata majeraha mabaya huko maaskari wake wawili wakiuawa.


Mashambulio yalioitikisa mji wa Bosaso jana usiku ilisikika maeneo mengi ya mitaa ya mji huo ambao walimwagwa wanamgambo wanaojulikana PIS ambapo ni maalum kwa mapambano dhidi ya kile kinchoitwa Ugaidi.


Vikosi vya Mujahidina wa Milima ya Golis wamefanya mashambulio kadhaa kwenye maeneo maalum ya mji wa Bosaso ingawa mashambulio ya jana usiku hakuna aliyedai kuhusika.

Post a Comment

 
Top