0


Kuna maelezo zaidi yameptikana kuhusiana na milipuko mikubwa yaliowalenga wanajeshi wa AMISOM kwenye mji wa Marka makao makuu ya mkoa wa Lower Shabelle.



Habari kutoka mji wa Marka zinathibitisha kuwa wanajeshi wa AMISOM wamekutana na milipuko miwili mikubwa yaliofuatana ndani ya mji wa Marka wakati walipokuwa wakichota maji mmoja ya visima wa mji huo.




Mashuhuda wamesema milipuko hizo imewazingira wanajeshi waliokuwa wakitembea kwa miguu na mmoja ya Magari ya kijeshi,vishindo vya milipuko hizo zilisikika ndani na nje ya mji wa Marka.



Duru zinaeleza kuwa Wanajeshi watatu wa Burundi walio sehemu ya wanajeshi wavamizi wa AMISOM wameuawa kwenye milipuko hizo,habari zaidi zinaeleza kuwa Baada ya tukio hilo wanajeshi hao Maadui walimpiga risasi mmoja wa wananchi alipokuwa akitembea katikati ya barabarani wa Marka.



Hali katika mji wa Marka ambao kwa muda wa masaa kadhaa ilikuwa katika hali ya tahruki kwa sasa iko shwari huko wanajeshi wa Kigeni wa AMISOM wakirusha Mizinga mikubwa upande wa Kaskazini mwa mji huo

Post a Comment

 
Top