0


Serikali ya Kenya imetangaza kuwa iko tayari kufanya mazungumzo na Harakat Al-Shabab Al Mujahideen inayoendesha harakati zake nchini Somalia na ndani ya Ardhi ya Kenya.



Kiongozi wa waliowengi katika Bunge la Kenya Adan Barre Duale amesema akiwa katika mji wa Garisa kuwa Kenya inataabika na mashambulio ya mara kwa mara kutoka kwa Harakat Al-Shabab Al Mujahideen na kwa hivyo basi hakuna budi kufanya mazungumzo nao.




"Tuko tayari kufanya mazungumzo na Al-Shabab tutawatumia viongozi wa Kidini na watuambie tu mahali waliko",alisema Adan Barre.



Amesema Jamii ya kisomali waliopo nchini Kenya hawakuwaradhi Uvamizi wa wanajeshi wake kuingia nchini Somalia,Vikosi vya Harakat Al-Shabab Al Mujahideen vimekuwa vikiendesha mashambulio ya mara kwa mara katika miji mikubwa nchini Kenya.



Haifahamika uwezekano wa kufanyika Mazungumzo kati ya Mujahidina wa Somalia na Serikali ya Kenya ambao wanajeshi wake wapo katika uvamizi nchini Somalia.

Post a Comment

 
Top