0
Watu waliokuwa wamejihami na silaha wamemwua Afisa wa Serikali shirikisho ya Somalia FG kwenye Wilaya ya Daniile mjini Mugadishu.



Walioshuhudia wanasema watu waliokuwa na silaha za Pisto walimpiga risasi mkuu wa Michezo katika Utawala wa Mungaabo Wilayani Dayniile,Afisa huyo aliyeuawa alishawahi kulengwa mara kadhaa na kunusurika kwenye mashambulio hayo yaliolenga kummaliza.




Upande mwingine watu waliokuwa na silaha walimpiga risasi na kumwua papo hapa mjini Marka Afisa mmoja wa kitengo cha  Ujasusi wanaojulikana PS ambao husaidiana na wavamizi wa Misalaba waliojiita AMISOM.



Katika miezi ya hivi karibuni mauaji inayowalenga maofisaa wa Serikali Shirikisho ya Somalia FG yameongezeka katika mji wa Mugadishu na mikoa mengine nchini Somalia.

Post a Comment

 
Top