0
Kocha Arsene Wenger pamoja na klabu ya Arsenal imepata pigo baada ya kiungo wake, Mesut Ozil kuumia na atakuwa nje kwa zaidi ya wiki 12 hivyo atakuwa nje kwa kipidi chote kilichobaki kumaliza mwaka 2014.
Mesut-Ozil-Arsenal-2245395
Kiungo huyo alikwenda kufanyiwa vipimo vya MRI katika goti lake na chama cha soka nchini Ujerumani ambacho kimethibitisha atakuwa nje kwa miezi mitatu. Kiungo huyo, 25, ambaye anaichezea Ujerumani, alicheza dakika 90 katika mechi ya Arsenal 0-2 Chelsea siku ya Jumapili.
Habari za kuumia kwake zinazokuja mwezi wa pili ndani ya msimu mpya, ni pigo kwa kocha Arsene Wenger ambaye sasa idadi ya majeruhi inaongezeka katika timu yake. Ozil akiungana na Aaron Ramsey, Mathieu Debuchy, Olivier Giroud pamoja na Mikel Arteta.

Post a Comment

 
Top