0
Muimbaji wa R&B anayetamba kwa sasa, August Alsina alijikuta akipata vifafa vya hapa na pale baada ya kuanguka wakati akitumbuiza jukwaani saa 24 zilizopita. Bado ameendelea kulazwa hospitali.
600_1395069716_august_alsina1_20
Mwakilishi wa msanii huyo ameuambia mtandao wa TMZ kuwa msanii huyo amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi jijini New York na anapewa matibabu ya kifafa. Alsina alizimia na kuanguka wakati akitumbuiza usiku wa jana jijini humo.
 
Amesema madaktari hawakukuta dawa zozote kwenye mwili wake zaidi ya bangi kwenye mfumo wake. Wanaamini kuzimia kwake kulitokana na kuchoka na kukosa maji.

Post a Comment

 
Top