Vifo zaidi ya 600 vimetokana na Ebola huko Afrika Magharibi.
Shirika la Afya Duniani WHO linasema kuwa idadi ya watu wanaofariki kutokana na mkurupuko wa maradhi ya Ebola katika maeneo ya Afrika magharibi, sasa imepanda na kufikia zaidi ya watu 600.
Maofisa wa matibabu wa kimataifa na wale wa maeneo hayo wanajaribu kuyafikia maeneo ya mataifa yaliyothirika na ugonjwa huo kama vile Guinea, Sierra Leone na Liberia.
Changamoto zachelesha udhibiti wa Ebola Afrika Magharibi
Ebola ni ugonjwa hatari unaosambaa kwa kasi mno hivyo huenda idadi kamili ya vifo vinavyotokana na Ebola isijulikane.
Baadhi ya waliowahi matibabu sahihi mapema wamepona.
Post a Comment