0
Dar es Salaam. Bodi ya Taifa ya Uhasibu (NBAA) imebadili mitalaa itakayotumika kuwatahini watahiniwa katika daraja juu la uhasibu Certified Public Accountant (CPA) kwa lengo la kuongeza ufanisi katika taaluma hiyo.
Mabadiliko hayo ya kimfumo yameenda sambamba na upunguzwaji wa masomo ili kwenda sambamba na mabadiliko ya mazingira, biashara na mwenendo ya ajira.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBBA, Pius Maneno alisema tofauti na ilivyokuwa awali mitaala hiyo mipya imeundwa kwa mfumo wa kuweza kutafsiri mafunzo kwa vitendo.
Alisema mfumo huo umelenga kumwelimisha mwanafunzi ili aweze kutumia mafunzo na kuimarisha ubora katika utendaji wa kazi ya uhasibu.
“Mitaala hii imekuja na mfumo tofauti kabisa na uliokuwa hapo awali, ambao ulikuwa umejikita zaidi kwenye usomaji wa nadharia ambao wengi walikuwa wanasoma kwa ajili ya kujibu mitihani, sasa mwanafunzi anapaswa kuwa na uelewa wa hali ya juu na kutafsiri mafunzo kwa vitendo,” alisema Maneno.
Mmoja wa wanafunzi waliojisalili kufanya mitihani hiyo Novemba mwaka huu Julius Nyirenda alisema mabadiliko hayo yanaleta unafuu kwa wanafunzi na kutoa hamasa ya wengi kufanya mitihani hiyo.
“Ni mfumo utakaowahamasisha wanafunzi wengi,”alisema.

Post a Comment

 
Top