0
Tarime. Waziri ya Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe amesema hatamvumilia askari yeyote anayefanya kazi kinyume na taaluma yake, badala ya kuwalinda wananchi na mali zao.
Chikawe alitoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani Tarime juzi, ikiwa na lengo la kujionea hali halisi yamalalamiko yaliyopelekwa kwake na kupitia wabunge.
Alisema wizara yake imedhamiria kuwashughulikia polisi wanaowanyanyasa wananchi, ili kurejesha imani ya raia wanaoumizwa kila siku na kubambukiwa kesi.
“Wizara yangu haitavumilia askari yeyote atakayefanya kazi ya kubabaisha, tunataka polisi wote wafanye kazi yao kitaaluma... hatuwezi kuwa askari ambao ni wahalifu,” alisema Waziri Chikawe.
Hata hivyo, Waziri Chikawe alisema hayo baada ya kupata taarifa kutoka wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa African Barrick Gold North Mara Nyamongo kuwa, kazi inayofanywa na polisi siyo ya ulinzi bali ujambazi.
Waziri Chikawe alisema kwamba yeye siyo mtu wa maneno bali vitendo, hivyo wategemee kuona wanaokiuka maadili ya kazi yao wakiwajibishwa kama ilivyoanza mikoa ya Shinyanga na Mara.
“Mimi siyo mtu wa maneno, bali ni vitendo na mtaona tayari baadhi ya wale wanaonekana kwenda kinyume na maadili hatua za kisheria zimeanza kuchukua mkondo wake,” alisema.
Licha ya tuhuma hizo, wananchi waliitupia lawama Serikali kwa kuwatelekeza bila kuwawekea miundombinu mizuri kwa ajili ya kutatua matatizo na migogoro inayoibuka kwenye jamii.
“Mwekezaji hana tatizo, maana wakati mwingine anafanya kazi za kujitolea, Serikali ndiyo imewatelekeza wananchi kwa kuwaacha wahangaike huku wakituhumiwa kuwa wanafichwa vigumu,” alisema Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyangoto, Elisha Nyamohanga.
Alisema viongozi wa ngazi za juu wanafanya ziara bila kushirikisha viongozi wa ngazi ya chini.
, hali inayosababisha wasipate kwa uhakika kero za wananchi.
“Hatukupata taarifa ya ujio wako hapa tumeshtushwa tu hapa, hakunadiwani, wenyeviti wa vitongoji na vijiji hata mbunge hatumwoni hapa,hali inayotuonyesha kuwa hamtujali,” alisema Nyamohanga.
Nyamohanga alitoa wito kuwa, ili kupunguza matatizo yaliyopovijiji vinavyozunguka mgodi huo Serikali iandae maeneo kwa wachimbaji wadogo na kuwapa vitendea kazi.
“Tatizo la mauaji hapa Nyamongo halitaisha iwapo Serikali haitaonaumhimu wa kuwapa wachimbaji wadogo maeneo yao, kwaniwanategemea uchimbaji wa dhahabu kama sehemu ya kipato chao,” alisema. Hata hivyo, Waziri Chikawe alisema ziara yake haikuwa ya utekelezaji, bali ni kujifunz kuona kile kinachomfikia ofisini ajue sehemu ya kuanzia.

Post a Comment

 
Top