MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji amevunja ukimya na kujibu
tuhuma zote zinazoikabili klabu, lakini akampa masharti mawili Emmanuel
Okwi raia wa Uganda anayeshinikiza uongozi ummalizie dola zake 40,000 za
usajili ili aendelee na kazi.
Yanga ilimsajili Okwi kwa ahadi ya kumpa dola
100,000 lakini ikampa dola 60,000 na kuahidi kumalizia baadaye. Manji
amesema, Okwi alisajiliwa klabuni hapo kwa mkataba wa miaka miwili na
nusu na walikuwa na makubaliano ambayo moja kati ya jukumu lake ilikuwa
ni kufuatilia kibali cha kumruhusu kucheza mpira Yanga.
Lakini kibali hicho kilichelewa akakosa baadhi ya
mechi za awali, pia akajitoa kwenye timu bila ruhusa maalumu hivyo
anachotakiwa ni kukatwa sehemu ya pesa zake za usajili au aongezewe muda
wa usajili uwe miaka mitatu.
“Majadiliano na Okwi yanaendelea
tutakachokubaliana na ndicho kitafanyika. Kama ilivyokuwa malengo yetu,
tulimsajili mchezaji huyo kwa ajili ya mashindano ya kimataifa,”alisema
Manji ambaye hana masihara linapokuja suala la fedha za klabu.
Kiongozi huyo atalitolea ufafanuzi zaidi suala la
yeye kutogombea Juni Mosi mwaka huu kwenye mkutano wa kurekebisha katiba
utakaofanyia Ukumbi wa Oysterbay Police Mess na mpango wake ni kuwa,
uchaguzi ufanyike Juni 15, mwaka huu.
Akitolea ufafanuzi suala la uchaguzi kuwahi, Manji
alisema; “Nimefanya hivi kwa ajili ya kutoa nafasi katika usajili.
Unajua kama tutachelewa na uongozi wa sasa ukafanya usajili inaweza kuwa
tatizo kwa mwingine unaokuja labda wachezaji tutakaowasajili sisi
litakuwa siyo chaguo lao.”
Kuhusu Domayo, Kavumbagu
Amesema, tangu Aprili hakuwepo nchini lakini
amesikia maneno mengi yanazungumzwa kuwa wamefanya uzembe kuwapoteza
wachezaji wawili, Frank Domayo na Mrundi Didier Kavumbagu.
“Ukweli ni kwamba, suala la Kavumbagu ilijulikana
awali msimu huu wachezaji wa kigeni ni watatu tu na tuliuliza TFF lakini
tatizo likaja, wakati tunajibiwa Kavumbagu alikuwa tayari amesajiliwa
na Azam,”alisema Manji na kusisitiza Kavumbagu alikuwa mchezaji mzuri
lakini watapata mwingine mzuri zaidi ya huyo.
“Kuhusu Domayo, kweli ni kijana mdogo tulifanya
uzembe kidogo hata hivyo, amekwenda Azam lakini atarudi Yanga kama
ilivyokuwa kwa Mrisho Ngassa.
Lakini akaenda mbali na kutupa dongo la baadhi ya viongozi ambao wanaponda juu ya hilo wakati wao ndiyo wana matatizo makubwa.
“Nimeongoza kwa miezi 19 lakini wapo walioongoza
nyuma yangu lakini hawakufanya kama mimi, walikuwa wanakimbia wanachama
na kutoitisha mikutano na wengine wanagombea uchaguzi mbalimbali lakini
wanashindwa.
“Nimesikia wanachama wanamfuata mwanachama mmoja awasaidie
kuongoza, kweli Yanga mmekosa wa kuwaongoza? Huyo mnayemfuata
tumemwandikia barua ya kulipa pesa za ahadi ya gari la usajili wa Ngassa
(Mrisho) ambayo alidai kutoa lakini hadi leo hii hajailipa,”alifafanua
Manji na kueleza juu ya kocha wao Mholanzi Hans Van Pluijm kuwa kabla ya
kuja Yanga walijua ataondoka.
“Nashangaa kauli ya kusema tunajenga uwanja kwenye
maji itakuwaje. Ndiyo tunapopataka hapohapo, tunayo mifano ya viwanja
vya nchi zilizoendelea kama Dubai, Uholanzi ambao wamejenga juu ya maji
kwa nini sisi tushindwe,”alihoji na kutolea mfano mwaka 1964 Serikali
yenyewe ilikuwa na mpango wa kujenga Uwanja wa Taifa hapohapo Jangwani.
Manji pia ametimua wanachama sita na kulifuta tawi
la Tandale. Wanachama Haji Kamtange, Waziri Jitu, Athuman Matandula,
Islael Dude, Mohamed Ndomba na Seleman Hassan ndiyo waliofutwa uanachama
kwa sababu walizungumza na vyombo vya habari kinyume na taratibu.
Pia amelifuta tawi la Tandale ambalo linachochea vurugu na uvunjaji amani kwenye klabu.
Post a Comment