0


Kumekua na wasiwasi wa ID Privacy kuhusiana na maamuzi ya kampuni kubwa ya Teknolojia Apple kuzindua Teknolojia ya Fingerprint kwa ajili ya kuifungua loki [unlock] simu hio, mjadala huo umetokea kwasababu wadau mbali mbali wa matumizi ya teknolojia kuhofia utambulisho wao/ID kuhifadhiwa na kutumika katika maswala ya ujasusi/spying. 
Lakini kampuni hio ya Apple imesema kwamba toleo lao hilo jipya la iPhone 5s haitakua ikihifadhi utambulisho wa alama za viganja/vidole katika simu hizo na kuwa wasiwe na wasiwasi kwa kua wanaheshimu na wanatambua umuhimu wa usiri/Privacy wa wateja wao. 
 Pia wamesema Teknolojia hio inachukua tu baadhi ya alama za vidole na ambayo ni simu peke yake ndo itaweza kumtambua mtumiaji wake, na pia Kampuni ya apple imesema kwamba teknolojia hio haitakua ikifanya kazi kwa ufasaha mda wote na hio nimoja ya udhaifu wake na pia haitakua na uwezo wa kusupport program nyingine zaidi ya za Apple tu.

Post a Comment

 
Top