Ikiwa na kichwa cha habari kisemacho "Ajira ya Watoto katika Migodi",
ripoti hiyo imefichua vitendo vya dhuluma na ukatili wanaokutana nao
watoto wao ambao baadhi yao wako hatarini kuangukia kwenye matatizo ya
kiafya ikiwemo mtindio wa ubungo kutokana na kemikali zinazokutikana
kwenye machimbo hayo.
Ripoti hiyo iliyotangazwa leo jijini Dar es salaam inafuatia utafiti
uliofanyika katika maeneo ya machimbo ambako watoto wengi wameajiriwa.
Maafisa wa Human Rights Watch wamesema kuwa pamoja na kutumika katika
kazi ngumu ya utafutaji madini, lakini baadhi ya watoto hao wanalazimika
kutumika katika biashara za kingono na kukubwa na matukio ya
unyanyasaji wa kijinsia.
Ripoti hiyo ambayo pia imeangazia athari zitokanazo na matumizi
ya madini ya zebaki kwenye machimbo hayo, imesema kuwa baadhi ya
kampuni binafsi na vikundi vya watu huwatumia watoto hao kusaka madini
jambo ambalo linakwenda kinyume na sheria za kimataifa.
Akiwasilisha ripoti hiyo, Mtafiti mkuu wa Human Watch, Jenina Morna,
alisema kuwa idadi kubwa ya watoto hao hufanya kazi kwenye mazingira
magumu na wakati mwingine hulazimika kuingia kwenye mapango yaliyoko
chini kwa chini kwa ajili ya kusaka madini.
"Watoto hufanya kazi katika migodi yenye kina kirefu mno, watoto hawa
husafirisha mizigo mizito ya dhahabu, na wakati mwingine hutumia vifaa
hararishi kusaka madini kama vile mawe." Alisema Morna.
Moja ya sababu kubwa inayowasuma watoto wengi kuingia kwenye migodi ni
hali ya kipato duni iliyopo kwenye familia nyingi, kama inavyothibitika
katika makala fupi iliyoandaliwa na Human Watch ikionyesha kina mama na
watoto wakihangaika na maisha.
Kwa sasa Tanzania ni nchi ya tatu barani Afrika kwa kuzalisha kwa wingi
madini ya dhahabu, ikizidiwa na nchi za Afrika ya Kusini na Ghana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment