Hivi karibuni kumekuwa na midahalo mbalimbali ambayo imekua ikiendelea katika nchi nyingi, ikiwamo Tanzania kuhusu masuala ya ulinzi wa huduma za mtandao.
Binafsi nimepata kuhudhuria mijadala kama
mwanachama wa kudumu wa kikundi kinachojihusisha na masuala ya ulinzi
mtandao katika nchi za Afrika.
Katika vikao tofauti, majadiliano yalikua ni mengi
ambapo hali ya usalama wa kimtandao imechambuliwa kwa ngazi ya kidunia,
na kudhihirika kuwa kumekuwepo na ongezeko kubwa la makosa ya
kimtandao, hususan mwaka huu.
Hadi sasa baadhi ya nchi tayari zimeweza kupiga
hatua katika kukabiliana na hali hiyo. Taarifa iliyowasilishwa na
Profesa Hamadoun Toure kutoka ITU (International Telecommunication
Union) iliyo chini ya Umoja wa Kimataifa ilisema, kuna mategemeo
mwishoni mwa mwaka huu pakawa na watumiaji biilioni 2.7 wa mtandao
Aidha, ripoti iliyowasiilishwa na ITU huko Geneva
ilisema, kumekuwepo na ongezeko kubwa la madhara ya uhalifu wa
kimtandao, ambapo ilielezwa mitandao imekuwa ikiathiriwa kwa zaidi ya
asilimia 30.
Pia mitandao ijulikanayo kama “Phishing Sites
spoofing social networks” imeongezeka kwa asilimia 125, na kuelezwa nusu
ya vijana wenye umri kati ya miaka 13 hadi 17 uliimwenguni kote wamekua
wakiathirrika na kilichotambulishwa kama “Cyberbulling”.
Vile vile tafiti zilizowasilishwa katika ripoti ya
“The World Federation of Exchanges and the International Organization
of Securities Commissions” zimeeleza nusu ya taasisi za fedha duniani
zimeweza kuathirika na uhalifu wa kimtandao ikiwamo wizi hadi kufikia
mwaka jana mwishoni
Kibaya zaidi ni kwamba takriban robo ya taasisi hizo zinaelezwa kushindwa kutatua changamoto hiyo.
Kimsingi, jambo hili na mengine yaliyojadiliwa kwa
kina yalionekana kuwa ni changamoto kubwa katika dunia ya sasa, ambapo
kutakuwa na ugumu mgumu kukimbia utumiaji wa teknolojia katika maisha ya
kila siku.
Hali ilivyo Tanzania
Kwa sasa hali ya utumiaji wa mitandao nchini
imeongezeka katika sekta mbalimbali, kuanzia kufanya miamala ya biashara
hadi katika sekta za elimu na maeneo mengine mengi.
Post a Comment