According to a report by Computerworld,
hackers have been storing Windows XP zero-day vulnerabilities that they
have discovered, with the intent of unleashing them on XP users the
moment Microsoft ceases extended support for the aging operating
system on April 8, 2014.
Hackers are reluctant to unleash the viruses now,
because exploits exposed now would be fixed in patches released to XP
users quickly. However, once support for the operating system stops,
users will no longer receive such updates.
Computerworld also projected that by April 8, 2014,
an astounding 33% - 34% of the world's computers will still be running
Windows XP, which would provide hackers with enough incentive to release
the viruses, as the potential for damage would be massive.
There are also some experts that say Microsoft will
be forced to provide support for Windows XP users. That's because if all
XP users were the target of a denial-of-service attack, the Internet
(which the XP machines are connected to) would be affected to a large
degree as well.
Another option for Microsoft, said Fossen, would be to
take advantage of a post-retirement disaster to do what it's been doing
for years, push customers to upgrade.
Tech savvy users would have switched to newer versions of Windows by
now, but there are some users or enterprises that insist on sticking
with Windows XP due to legacy software or for financial reasons. If your
company or someone you know is using Windows XP, now would be a good
time to convince them to upgrade to either Windows 7 or Windows 8.Kinachosemwa, na Ukweli kuhusu Sera ya Mtoto Mmoja nchini China
Sera ya uzazi wa mpango ya China, maarufu kama sera ya mtoto mmoja, ni
sera inayofahamika sana duniani kwanza kutokana na ufanisi wake katika
kudhibiti ongezeko la idadi ya watu, na pili kutokana na kupata upinzani
mkali kutoka kwa baadhi ya taasisi za kidini nje ya China. Lakini
pamoja na sera hiyo kufahamika kutokana na sababu hizo mbili, bado watu
walio nje ya China wana uelewa mdogo sana kuhusu undani wa sera hii, na
hawajui inatekelezwa vipi, ina manufaa gani na changamoto gani, na nini
tunaweza kujifunza kutokana na sera hii.
Sera ya uzazi wa mpango ya China ilianza kutekelezwa miaka 70 karne iliyopita, ili kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu. Kimsingi sera hii inawataka kila wanandoa wachina wawe na mtoto mmoja. Nimeamua kutumia neno “kimsingi” kwa kuwa si wanandoa wote wanaotakiwa au wanaolazimishwa kuwa na mtoto mmoja kama baadhi ya watu wanavyoambiwa na kuamini.
Sera hii kwanza inawalenga watu wa kabila kubwa zaidi la China, yaani wa-Han, ambao wanachukua zaidi ya 95 ya idadi ya watu wote wa China. Watu wa makabila mengine ambayo nchini China yanaitwa makabila madogo madogo wanaweza kutekeleza sera hiyo kwa hiari, na baadhi yao hata wanapewa ruzuku kutokana na kufuata sera hiyo kwa hiari. Hata hao wa-han si wote wanaotakiwa kutekeleza sera hiyo kama sera inavyoelezwa, kuna wakati baadhi hawabanwi sana na sera hiyo.
Kwa mfano, wa-han wachina wanaoishi vijijini wanaotegemea shughuli za kilimo, sera hii haiwabani sana kwa kuwa wanahitaji nguvu zaidi, kwa hiyo wanaweza kuwa na mtoto zaidi ya mmoja. Wa-han wa mijini ambao wote ni mtoto pekee kwenye familia zao, wakioana wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Wa-han wanaobanwa na sera hii wakienda kinyume wanatozwa faini. Kwa hiyo ukiangalia vizuri unaweza kuona kuwa, kwa wachina wa kabila la wa-han sera hii ni kama sheria, lakini kwa wachina wa makabila mengine ni sera ambayo utekelezaji wake ni hiari.
Hebu kwanza tutupie macho hali nchini China katika miaka ya 1970 wakati ilipoamua kutekeleza sera ya uzazi wa mpango. Jamhuri ya watu wa China ilianzishwa mwaka 1949 baada ya mapigano na vita vilivyodumu kwa karibu miaka 100 nchini China. Mwaka 1949 idadi ya wachina ilikuwa milioni 550, na kwa wastani watu waliokuwa wanaishi miaka 35. Lakini hadi kufikia mwaka 1980, idadi ya watu wa China iliongezeka na kufikia bilioni 1 na umri wa wastani wa maisha ya mchina pia uliongezeka na kufikia miaka 68. Kutokana na makadirio yaliyofanyika mwaka 1980, idadi ya watu wa China ingeweza kufikia bilioni 1.4 hadi ifikapo mwaka 2000.
Ukiangalia sababu nyingi zilizowafanya wachina waanze kutekeleza sera hii, unaweza kuona kuwa kuna mazingira mengi yanayofanana na hali ya sasa ya Tanzania. Idadi kubwa ya watu ni shinikizo kubwa sana kwa maliasili na raslimali za jamii kama vile ardhi, maji, chakula, shule, hospitali na miundo mbinu mingine. Mwanzoni mwa miaka ya sabini changamoto hizo zilikuwa ni mzigo mkubwa sana kwa wachina, na ni changamoto hizo hizo ambazo kwa sasa sisi watanzania tunalalamika nazo kila kukicha. Lakini changamoto hizo hazipo kwa Tanzania peke yake, bali pia zipo katika maeneo mengine duniani, ambako maliasili zinaendelea kupungua.
Nchini China watu walijua kuwa kama wakiendelea kuzaliana kwa wingi, basi ingekuwa ndoto au ingechukua muda mrefu kuwa na ongezeko la uchumi, na hata kama kungekuwa na ongezeko lolote la uchumi, ongezeko hilo lingefutwa na ongezeko la idadi ya watu. Kwa sasa hapa Tanzania tunasema kasi ya uchumi wa nchi yetu inaongezeka kwa asilimia zaidi ya 5 na 6 hivi. Hii kwa kweli ni habari nzuri, lakini ongezeko hilo halionekani kwenye maisha ya mtanzania wa kawaida, inawezekana kuwa ongezeko hilo linafutwa na ongezeko la idadi ya watu.
Hata tukiangalia familia moja moja, ni wazi kuwa ukiwa na watoto wengi kuliko uwezo wako wa kuwamudu, kwanza kama mzazi utatumia muda mwingi kujaribu kuwatunza watoto wako, na pili unaweza kukosa muda wa kutosha kutumia akili zako na nguvu zako kufanya mambo mengine yanayoweza kukunufaisha wewe na kulinufaisha taifa.
Mbali na maelezo yanayotolewa na serikali ya China kuhusiana na manufaa ya kiuchumi yanayotokana na utekelezaji wa sera hii, ukiwauliza wachina wa kawaida hasa wa mijini, wanakwambia kuwa hata kama isingekuwa sera ya serikali, wengi wao wanalazimika kutekeleza sera hiyo kutokana na mazingira ya sasa ya kiuchumi. Si rahisi kumudu kununua nyumba ya kuwatunza watoto watano, si rahisi kununua chakula cha kuwalisha watoto wengi namna hiyo, na zaidi ni vigumu sana kumudu gharama za elimu, matibabu na huduma nyingine kwa ajili ya watoto. Kwa ufupi ni kwamba, kuwa na idadi kubwa ya watoto, kwa mazingira ya nchi kama China, hasa mijini, ni kujiletea matatizo makubwa.
Hata hivyo sera yoyote lazima iendane na hali halisi. Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na ongezeko la uchumi na kuinuka kwa kiwango cha maisha, wachina hasa wakazi wa mijini katika maeneo yaliyoendelea kiuchumi, wanandoa vijana wanaonesha nia ya kuahirisha umri wa kuzaa mtoto, na baadhi yao kuamua kutooana au kutozaa.
Kwa upande mwingine wazee wanaishi kwa muda mrefu zaidi, hali ambayo inafanya kuwe na wazee wengi katika jamii ya China. Ndiyo maana pamoja na kuendelea na juhudi za kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu, serikali ya China imeanza kufikiria na kuchukua hatua ya kurekebisha sera yake ya uzazi wa mpango. Hatua moja ni kwamba, wanandoa ambao wao ni mtoto pekee kwenye familia, wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Na serikali pia ilichagua baadhi ya maeneo kufanya jaribio la watoto wawili, lakini watu wengi waishio maeneo hayo hawapendi kuzaa mtoto zaidi ya mmoja, tofauti na ilivyodhaniwa. Kuna wachina wengi tu ambao wanaamua kuoana na kutozaa, labda kutokana na utamaduni wa sisi waafrika jambo hili halifikiriki.
Pamoja na kuwa sera hii imeshambuliwa na jumuiya za haki za binadamu duniani na taasisi za kidini, hasa kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya utoaji mimba hasa inapojulikana kuwa ni mtoto wa kike, na kutokana na kinachotajwa kuwa ni kuzuia uhuru wa mtu kuamua idadi ya watoto anaotaka, lakini tukiangalia lengo la kimsingi la uwepo wa sera hii—kulinganisha matokeo ya uzalishaji wa mtu mmoja moja na thamani ya uzalishaji wa mali na maendeleo ya uchumi na jamii kwa ujumla, tunaweza kusema sera hii kimsingi imekuwa na manufaa kwa mtu mmoja mmoja, familia na nchi kwa ujumla.
Inakadiriwa kuwa sera hii imepunguza ongezeko la idadi ya watu kwa watu milioni 400, maana yake ni kuwa maliasili na rasilimali ambazo zingetumika kwa ajili ya watu hao milioni 400, sasa zinatumika kuboresha maisha ya watu waliopo sasa. Afya ya kina mama wanaojifungua na huduma wanazopata wakati wa kujifungua vyote vimeboreshwa, na kutokana na kutokuwa wajawazito mara kwa mara, kina mama wanashiriki zaidi kwenye shughuli za uchumi, na hata watoto wanakuwa na afya zaidi, mazingira mazuri zaidi ya elimu na hata kuwa na mustakbali mzuri zaidi.
Tanzania tumewahi kuwa na kampeni kubwa iliyokuwa inatoa mafunzo mazuri sana kuhusu afya ya uzazi na hata manufaa yake kwa mlengwa, ikishirikisha taasisi zisizo za kiserikali. Pamoja umuhimu wake, kampeni hiyo ilikosolewa na baadhi ya taasisi za kidini, lakini ilionesha mwelekeo mzuri. Sijui kwa sasa Chama Cha Uzazi wa Mpango na Malezi bora UMATI kilichokuwa kinahimiza kampeni hiyo kinachukuliwa vipi, kina mwelekeo gani na kina uwezo gani wa kuhimiza upangaji wa sera za taifa kwenye mambo ya uzazi na kusimamia utekelezaji wake. Kama Chama hiki kikipewa msukomo zaidi wa kufanya kazi na kuwafikia watanzania wengi, kuna uwezekano kuwa chama hiki kitakuwa ni jibu la tatizo la ongezeko la idadi ya watu Tanzania. Kwa kuwa chama hiki kinajua vizuri mazingira ya watanzania kiuchumi, kidini na hata mienendo ya uzazi ya watanzania.
Hapa Tanzania changamoto ya idadi ya watu, haitazamwi kwa umakini unaostahili. Pamoja na kuwa kuna baadhi ya watu wanazungumza suala hilo, inaonekana kuwa lipo vinywani tu. Bado baadhi yetu tunaamua tu kuzaa kwa kuwa tumefikisha umri fulani, sio kwa kuwa kweli tunahitaji kuwa na watoto, uwezo wa kukabiliana na majukumu ya kuwa na mtoto au sisi wenyewe kuwa wazazi, au tunaiga mkumbo na kuchagua kuwa na idadi ya watoto tunaopenda kuwa nao bila kuzingatia kama tuna uwezo wa kuwatunza na kuwawezesha waishi maisha bora, na baadhi tunachukulia fahari na kuona ni jambo la kawaida kuwa na watoto nje ya ndoa, kuwatelekeza na kuwafanya wengine wawe watoto wa mitaani. Ni kawaida kuona mtu ana watoto watano, lakini kimsingi hana hata uwezo wa kiuchumi wa kumudu kumtunza mtoto mmoja, lakini ukiuliza ni kwanini ana watoto wengi, huwezi kupata jibu la maana, zaidi ya kusema Mungu atawaangalia.
Sera ya mtoto mmoja ya China ina dosari zake, na wachina wenyewe wanajua dosari hizo, na kwa sasa kuna mjadala unaoendelea kuhusu kuifanyia mabadiliko sera hiyo ili iendane na mazingira ya sasa. Siwezi kusema kuwa sera hiyo inafaa kwa Tanzania au la, kwa kuwa kuna mambo mengi yanaoendana na sera hiyo ambayo yako kinyume kabisa na maadili, utamaduni na mazingira ya Tanzania. Lakini pia kuna mambo mengi yaliyomo kwenye sera hiyo, ikiwa ni pamoja na mantiki ya sera yenyewe, yanayoweza kuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania na watanzania.
Ni bora kuwepo na sera ya maana inayotekelezwa na kulalamikwa, kuliko kutokuwa kabisa na sera au kuwa sera midomoni na kwenye makaratasi tu, na kuacha ongezeko la idadi ya watu liendelee kuwa bomu linalokaribia kulipuka.
Tunachotakiwa kukumbuka ni kuwa, sera inayohusu idadi ya watu ni sera muhimu kwa taifa inayopaswa kupangwa kwa uangalifu sana tangu mwanzo, kwani athari au manufaa yake hayaonekani mara moja, lakini hakika sera ya namna hiyo inaweza kuwa na manufaa kwa taifa pamoja na mwananchi mmoja mmoja baada ya miaka 10 hadi 20, wakati watu wa kizazi kimoja watakapokuwa wamekua, kuingia kwenye soko la ajira na kutaka maisha bora.
Sera ya uzazi wa mpango ya China ilianza kutekelezwa miaka 70 karne iliyopita, ili kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu. Kimsingi sera hii inawataka kila wanandoa wachina wawe na mtoto mmoja. Nimeamua kutumia neno “kimsingi” kwa kuwa si wanandoa wote wanaotakiwa au wanaolazimishwa kuwa na mtoto mmoja kama baadhi ya watu wanavyoambiwa na kuamini.
Sera hii kwanza inawalenga watu wa kabila kubwa zaidi la China, yaani wa-Han, ambao wanachukua zaidi ya 95 ya idadi ya watu wote wa China. Watu wa makabila mengine ambayo nchini China yanaitwa makabila madogo madogo wanaweza kutekeleza sera hiyo kwa hiari, na baadhi yao hata wanapewa ruzuku kutokana na kufuata sera hiyo kwa hiari. Hata hao wa-han si wote wanaotakiwa kutekeleza sera hiyo kama sera inavyoelezwa, kuna wakati baadhi hawabanwi sana na sera hiyo.
Kwa mfano, wa-han wachina wanaoishi vijijini wanaotegemea shughuli za kilimo, sera hii haiwabani sana kwa kuwa wanahitaji nguvu zaidi, kwa hiyo wanaweza kuwa na mtoto zaidi ya mmoja. Wa-han wa mijini ambao wote ni mtoto pekee kwenye familia zao, wakioana wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Wa-han wanaobanwa na sera hii wakienda kinyume wanatozwa faini. Kwa hiyo ukiangalia vizuri unaweza kuona kuwa, kwa wachina wa kabila la wa-han sera hii ni kama sheria, lakini kwa wachina wa makabila mengine ni sera ambayo utekelezaji wake ni hiari.
Hebu kwanza tutupie macho hali nchini China katika miaka ya 1970 wakati ilipoamua kutekeleza sera ya uzazi wa mpango. Jamhuri ya watu wa China ilianzishwa mwaka 1949 baada ya mapigano na vita vilivyodumu kwa karibu miaka 100 nchini China. Mwaka 1949 idadi ya wachina ilikuwa milioni 550, na kwa wastani watu waliokuwa wanaishi miaka 35. Lakini hadi kufikia mwaka 1980, idadi ya watu wa China iliongezeka na kufikia bilioni 1 na umri wa wastani wa maisha ya mchina pia uliongezeka na kufikia miaka 68. Kutokana na makadirio yaliyofanyika mwaka 1980, idadi ya watu wa China ingeweza kufikia bilioni 1.4 hadi ifikapo mwaka 2000.
Ukiangalia sababu nyingi zilizowafanya wachina waanze kutekeleza sera hii, unaweza kuona kuwa kuna mazingira mengi yanayofanana na hali ya sasa ya Tanzania. Idadi kubwa ya watu ni shinikizo kubwa sana kwa maliasili na raslimali za jamii kama vile ardhi, maji, chakula, shule, hospitali na miundo mbinu mingine. Mwanzoni mwa miaka ya sabini changamoto hizo zilikuwa ni mzigo mkubwa sana kwa wachina, na ni changamoto hizo hizo ambazo kwa sasa sisi watanzania tunalalamika nazo kila kukicha. Lakini changamoto hizo hazipo kwa Tanzania peke yake, bali pia zipo katika maeneo mengine duniani, ambako maliasili zinaendelea kupungua.
Nchini China watu walijua kuwa kama wakiendelea kuzaliana kwa wingi, basi ingekuwa ndoto au ingechukua muda mrefu kuwa na ongezeko la uchumi, na hata kama kungekuwa na ongezeko lolote la uchumi, ongezeko hilo lingefutwa na ongezeko la idadi ya watu. Kwa sasa hapa Tanzania tunasema kasi ya uchumi wa nchi yetu inaongezeka kwa asilimia zaidi ya 5 na 6 hivi. Hii kwa kweli ni habari nzuri, lakini ongezeko hilo halionekani kwenye maisha ya mtanzania wa kawaida, inawezekana kuwa ongezeko hilo linafutwa na ongezeko la idadi ya watu.
Hata tukiangalia familia moja moja, ni wazi kuwa ukiwa na watoto wengi kuliko uwezo wako wa kuwamudu, kwanza kama mzazi utatumia muda mwingi kujaribu kuwatunza watoto wako, na pili unaweza kukosa muda wa kutosha kutumia akili zako na nguvu zako kufanya mambo mengine yanayoweza kukunufaisha wewe na kulinufaisha taifa.
Mbali na maelezo yanayotolewa na serikali ya China kuhusiana na manufaa ya kiuchumi yanayotokana na utekelezaji wa sera hii, ukiwauliza wachina wa kawaida hasa wa mijini, wanakwambia kuwa hata kama isingekuwa sera ya serikali, wengi wao wanalazimika kutekeleza sera hiyo kutokana na mazingira ya sasa ya kiuchumi. Si rahisi kumudu kununua nyumba ya kuwatunza watoto watano, si rahisi kununua chakula cha kuwalisha watoto wengi namna hiyo, na zaidi ni vigumu sana kumudu gharama za elimu, matibabu na huduma nyingine kwa ajili ya watoto. Kwa ufupi ni kwamba, kuwa na idadi kubwa ya watoto, kwa mazingira ya nchi kama China, hasa mijini, ni kujiletea matatizo makubwa.
Hata hivyo sera yoyote lazima iendane na hali halisi. Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na ongezeko la uchumi na kuinuka kwa kiwango cha maisha, wachina hasa wakazi wa mijini katika maeneo yaliyoendelea kiuchumi, wanandoa vijana wanaonesha nia ya kuahirisha umri wa kuzaa mtoto, na baadhi yao kuamua kutooana au kutozaa.
Kwa upande mwingine wazee wanaishi kwa muda mrefu zaidi, hali ambayo inafanya kuwe na wazee wengi katika jamii ya China. Ndiyo maana pamoja na kuendelea na juhudi za kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu, serikali ya China imeanza kufikiria na kuchukua hatua ya kurekebisha sera yake ya uzazi wa mpango. Hatua moja ni kwamba, wanandoa ambao wao ni mtoto pekee kwenye familia, wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Na serikali pia ilichagua baadhi ya maeneo kufanya jaribio la watoto wawili, lakini watu wengi waishio maeneo hayo hawapendi kuzaa mtoto zaidi ya mmoja, tofauti na ilivyodhaniwa. Kuna wachina wengi tu ambao wanaamua kuoana na kutozaa, labda kutokana na utamaduni wa sisi waafrika jambo hili halifikiriki.
Pamoja na kuwa sera hii imeshambuliwa na jumuiya za haki za binadamu duniani na taasisi za kidini, hasa kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya utoaji mimba hasa inapojulikana kuwa ni mtoto wa kike, na kutokana na kinachotajwa kuwa ni kuzuia uhuru wa mtu kuamua idadi ya watoto anaotaka, lakini tukiangalia lengo la kimsingi la uwepo wa sera hii—kulinganisha matokeo ya uzalishaji wa mtu mmoja moja na thamani ya uzalishaji wa mali na maendeleo ya uchumi na jamii kwa ujumla, tunaweza kusema sera hii kimsingi imekuwa na manufaa kwa mtu mmoja mmoja, familia na nchi kwa ujumla.
Inakadiriwa kuwa sera hii imepunguza ongezeko la idadi ya watu kwa watu milioni 400, maana yake ni kuwa maliasili na rasilimali ambazo zingetumika kwa ajili ya watu hao milioni 400, sasa zinatumika kuboresha maisha ya watu waliopo sasa. Afya ya kina mama wanaojifungua na huduma wanazopata wakati wa kujifungua vyote vimeboreshwa, na kutokana na kutokuwa wajawazito mara kwa mara, kina mama wanashiriki zaidi kwenye shughuli za uchumi, na hata watoto wanakuwa na afya zaidi, mazingira mazuri zaidi ya elimu na hata kuwa na mustakbali mzuri zaidi.
Tanzania tumewahi kuwa na kampeni kubwa iliyokuwa inatoa mafunzo mazuri sana kuhusu afya ya uzazi na hata manufaa yake kwa mlengwa, ikishirikisha taasisi zisizo za kiserikali. Pamoja umuhimu wake, kampeni hiyo ilikosolewa na baadhi ya taasisi za kidini, lakini ilionesha mwelekeo mzuri. Sijui kwa sasa Chama Cha Uzazi wa Mpango na Malezi bora UMATI kilichokuwa kinahimiza kampeni hiyo kinachukuliwa vipi, kina mwelekeo gani na kina uwezo gani wa kuhimiza upangaji wa sera za taifa kwenye mambo ya uzazi na kusimamia utekelezaji wake. Kama Chama hiki kikipewa msukomo zaidi wa kufanya kazi na kuwafikia watanzania wengi, kuna uwezekano kuwa chama hiki kitakuwa ni jibu la tatizo la ongezeko la idadi ya watu Tanzania. Kwa kuwa chama hiki kinajua vizuri mazingira ya watanzania kiuchumi, kidini na hata mienendo ya uzazi ya watanzania.
Hapa Tanzania changamoto ya idadi ya watu, haitazamwi kwa umakini unaostahili. Pamoja na kuwa kuna baadhi ya watu wanazungumza suala hilo, inaonekana kuwa lipo vinywani tu. Bado baadhi yetu tunaamua tu kuzaa kwa kuwa tumefikisha umri fulani, sio kwa kuwa kweli tunahitaji kuwa na watoto, uwezo wa kukabiliana na majukumu ya kuwa na mtoto au sisi wenyewe kuwa wazazi, au tunaiga mkumbo na kuchagua kuwa na idadi ya watoto tunaopenda kuwa nao bila kuzingatia kama tuna uwezo wa kuwatunza na kuwawezesha waishi maisha bora, na baadhi tunachukulia fahari na kuona ni jambo la kawaida kuwa na watoto nje ya ndoa, kuwatelekeza na kuwafanya wengine wawe watoto wa mitaani. Ni kawaida kuona mtu ana watoto watano, lakini kimsingi hana hata uwezo wa kiuchumi wa kumudu kumtunza mtoto mmoja, lakini ukiuliza ni kwanini ana watoto wengi, huwezi kupata jibu la maana, zaidi ya kusema Mungu atawaangalia.
Sera ya mtoto mmoja ya China ina dosari zake, na wachina wenyewe wanajua dosari hizo, na kwa sasa kuna mjadala unaoendelea kuhusu kuifanyia mabadiliko sera hiyo ili iendane na mazingira ya sasa. Siwezi kusema kuwa sera hiyo inafaa kwa Tanzania au la, kwa kuwa kuna mambo mengi yanaoendana na sera hiyo ambayo yako kinyume kabisa na maadili, utamaduni na mazingira ya Tanzania. Lakini pia kuna mambo mengi yaliyomo kwenye sera hiyo, ikiwa ni pamoja na mantiki ya sera yenyewe, yanayoweza kuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania na watanzania.
Ni bora kuwepo na sera ya maana inayotekelezwa na kulalamikwa, kuliko kutokuwa kabisa na sera au kuwa sera midomoni na kwenye makaratasi tu, na kuacha ongezeko la idadi ya watu liendelee kuwa bomu linalokaribia kulipuka.
Tunachotakiwa kukumbuka ni kuwa, sera inayohusu idadi ya watu ni sera muhimu kwa taifa inayopaswa kupangwa kwa uangalifu sana tangu mwanzo, kwani athari au manufaa yake hayaonekani mara moja, lakini hakika sera ya namna hiyo inaweza kuwa na manufaa kwa taifa pamoja na mwananchi mmoja mmoja baada ya miaka 10 hadi 20, wakati watu wa kizazi kimoja watakapokuwa wamekua, kuingia kwenye soko la ajira na kutaka maisha bora.
Kinachosemwa, na Ukweli kuhusu Sera ya Mtoto Mmoja nchini China
Sera ya uzazi wa mpango ya China, maarufu kama sera ya mtoto mmoja, ni
sera inayofahamika sana duniani kwanza kutokana na ufanisi wake katika
kudhibiti ongezeko la idadi ya watu, na pili kutokana na kupata upinzani
mkali kutoka kwa baadhi ya taasisi za kidini nje ya China. Lakini
pamoja na sera hiyo kufahamika kutokana na sababu hizo mbili, bado watu
walio nje ya China wana uelewa mdogo sana kuhusu undani wa sera hii, na
hawajui inatekelezwa vipi, ina manufaa gani na changamoto gani, na nini
tunaweza kujifunza kutokana na sera hii.
Sera ya uzazi wa mpango ya China ilianza kutekelezwa miaka 70 karne iliyopita, ili kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu. Kimsingi sera hii inawataka kila wanandoa wachina wawe na mtoto mmoja. Nimeamua kutumia neno “kimsingi” kwa kuwa si wanandoa wote wanaotakiwa au wanaolazimishwa kuwa na mtoto mmoja kama baadhi ya watu wanavyoambiwa na kuamini.
Sera hii kwanza inawalenga watu wa kabila kubwa zaidi la China, yaani wa-Han, ambao wanachukua zaidi ya 95 ya idadi ya watu wote wa China. Watu wa makabila mengine ambayo nchini China yanaitwa makabila madogo madogo wanaweza kutekeleza sera hiyo kwa hiari, na baadhi yao hata wanapewa ruzuku kutokana na kufuata sera hiyo kwa hiari. Hata hao wa-han si wote wanaotakiwa kutekeleza sera hiyo kama sera inavyoelezwa, kuna wakati baadhi hawabanwi sana na sera hiyo.
Kwa mfano, wa-han wachina wanaoishi vijijini wanaotegemea shughuli za kilimo, sera hii haiwabani sana kwa kuwa wanahitaji nguvu zaidi, kwa hiyo wanaweza kuwa na mtoto zaidi ya mmoja. Wa-han wa mijini ambao wote ni mtoto pekee kwenye familia zao, wakioana wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Wa-han wanaobanwa na sera hii wakienda kinyume wanatozwa faini. Kwa hiyo ukiangalia vizuri unaweza kuona kuwa, kwa wachina wa kabila la wa-han sera hii ni kama sheria, lakini kwa wachina wa makabila mengine ni sera ambayo utekelezaji wake ni hiari.
Hebu kwanza tutupie macho hali nchini China katika miaka ya 1970 wakati ilipoamua kutekeleza sera ya uzazi wa mpango. Jamhuri ya watu wa China ilianzishwa mwaka 1949 baada ya mapigano na vita vilivyodumu kwa karibu miaka 100 nchini China. Mwaka 1949 idadi ya wachina ilikuwa milioni 550, na kwa wastani watu waliokuwa wanaishi miaka 35. Lakini hadi kufikia mwaka 1980, idadi ya watu wa China iliongezeka na kufikia bilioni 1 na umri wa wastani wa maisha ya mchina pia uliongezeka na kufikia miaka 68. Kutokana na makadirio yaliyofanyika mwaka 1980, idadi ya watu wa China ingeweza kufikia bilioni 1.4 hadi ifikapo mwaka 2000.
Ukiangalia sababu nyingi zilizowafanya wachina waanze kutekeleza sera hii, unaweza kuona kuwa kuna mazingira mengi yanayofanana na hali ya sasa ya Tanzania. Idadi kubwa ya watu ni shinikizo kubwa sana kwa maliasili na raslimali za jamii kama vile ardhi, maji, chakula, shule, hospitali na miundo mbinu mingine. Mwanzoni mwa miaka ya sabini changamoto hizo zilikuwa ni mzigo mkubwa sana kwa wachina, na ni changamoto hizo hizo ambazo kwa sasa sisi watanzania tunalalamika nazo kila kukicha. Lakini changamoto hizo hazipo kwa Tanzania peke yake, bali pia zipo katika maeneo mengine duniani, ambako maliasili zinaendelea kupungua.
Nchini China watu walijua kuwa kama wakiendelea kuzaliana kwa wingi, basi ingekuwa ndoto au ingechukua muda mrefu kuwa na ongezeko la uchumi, na hata kama kungekuwa na ongezeko lolote la uchumi, ongezeko hilo lingefutwa na ongezeko la idadi ya watu. Kwa sasa hapa Tanzania tunasema kasi ya uchumi wa nchi yetu inaongezeka kwa asilimia zaidi ya 5 na 6 hivi. Hii kwa kweli ni habari nzuri, lakini ongezeko hilo halionekani kwenye maisha ya mtanzania wa kawaida, inawezekana kuwa ongezeko hilo linafutwa na ongezeko la idadi ya watu.
Hata tukiangalia familia moja moja, ni wazi kuwa ukiwa na watoto wengi kuliko uwezo wako wa kuwamudu, kwanza kama mzazi utatumia muda mwingi kujaribu kuwatunza watoto wako, na pili unaweza kukosa muda wa kutosha kutumia akili zako na nguvu zako kufanya mambo mengine yanayoweza kukunufaisha wewe na kulinufaisha taifa.
Mbali na maelezo yanayotolewa na serikali ya China kuhusiana na manufaa ya kiuchumi yanayotokana na utekelezaji wa sera hii, ukiwauliza wachina wa kawaida hasa wa mijini, wanakwambia kuwa hata kama isingekuwa sera ya serikali, wengi wao wanalazimika kutekeleza sera hiyo kutokana na mazingira ya sasa ya kiuchumi. Si rahisi kumudu kununua nyumba ya kuwatunza watoto watano, si rahisi kununua chakula cha kuwalisha watoto wengi namna hiyo, na zaidi ni vigumu sana kumudu gharama za elimu, matibabu na huduma nyingine kwa ajili ya watoto. Kwa ufupi ni kwamba, kuwa na idadi kubwa ya watoto, kwa mazingira ya nchi kama China, hasa mijini, ni kujiletea matatizo makubwa.
Hata hivyo sera yoyote lazima iendane na hali halisi. Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na ongezeko la uchumi na kuinuka kwa kiwango cha maisha, wachina hasa wakazi wa mijini katika maeneo yaliyoendelea kiuchumi, wanandoa vijana wanaonesha nia ya kuahirisha umri wa kuzaa mtoto, na baadhi yao kuamua kutooana au kutozaa.
Kwa upande mwingine wazee wanaishi kwa muda mrefu zaidi, hali ambayo inafanya kuwe na wazee wengi katika jamii ya China. Ndiyo maana pamoja na kuendelea na juhudi za kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu, serikali ya China imeanza kufikiria na kuchukua hatua ya kurekebisha sera yake ya uzazi wa mpango. Hatua moja ni kwamba, wanandoa ambao wao ni mtoto pekee kwenye familia, wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Na serikali pia ilichagua baadhi ya maeneo kufanya jaribio la watoto wawili, lakini watu wengi waishio maeneo hayo hawapendi kuzaa mtoto zaidi ya mmoja, tofauti na ilivyodhaniwa. Kuna wachina wengi tu ambao wanaamua kuoana na kutozaa, labda kutokana na utamaduni wa sisi waafrika jambo hili halifikiriki.
Pamoja na kuwa sera hii imeshambuliwa na jumuiya za haki za binadamu duniani na taasisi za kidini, hasa kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya utoaji mimba hasa inapojulikana kuwa ni mtoto wa kike, na kutokana na kinachotajwa kuwa ni kuzuia uhuru wa mtu kuamua idadi ya watoto anaotaka, lakini tukiangalia lengo la kimsingi la uwepo wa sera hii—kulinganisha matokeo ya uzalishaji wa mtu mmoja moja na thamani ya uzalishaji wa mali na maendeleo ya uchumi na jamii kwa ujumla, tunaweza kusema sera hii kimsingi imekuwa na manufaa kwa mtu mmoja mmoja, familia na nchi kwa ujumla.
Inakadiriwa kuwa sera hii imepunguza ongezeko la idadi ya watu kwa watu milioni 400, maana yake ni kuwa maliasili na rasilimali ambazo zingetumika kwa ajili ya watu hao milioni 400, sasa zinatumika kuboresha maisha ya watu waliopo sasa. Afya ya kina mama wanaojifungua na huduma wanazopata wakati wa kujifungua vyote vimeboreshwa, na kutokana na kutokuwa wajawazito mara kwa mara, kina mama wanashiriki zaidi kwenye shughuli za uchumi, na hata watoto wanakuwa na afya zaidi, mazingira mazuri zaidi ya elimu na hata kuwa na mustakbali mzuri zaidi.
Tanzania tumewahi kuwa na kampeni kubwa iliyokuwa inatoa mafunzo mazuri sana kuhusu afya ya uzazi na hata manufaa yake kwa mlengwa, ikishirikisha taasisi zisizo za kiserikali. Pamoja umuhimu wake, kampeni hiyo ilikosolewa na baadhi ya taasisi za kidini, lakini ilionesha mwelekeo mzuri. Sijui kwa sasa Chama Cha Uzazi wa Mpango na Malezi bora UMATI kilichokuwa kinahimiza kampeni hiyo kinachukuliwa vipi, kina mwelekeo gani na kina uwezo gani wa kuhimiza upangaji wa sera za taifa kwenye mambo ya uzazi na kusimamia utekelezaji wake. Kama Chama hiki kikipewa msukomo zaidi wa kufanya kazi na kuwafikia watanzania wengi, kuna uwezekano kuwa chama hiki kitakuwa ni jibu la tatizo la ongezeko la idadi ya watu Tanzania. Kwa kuwa chama hiki kinajua vizuri mazingira ya watanzania kiuchumi, kidini na hata mienendo ya uzazi ya watanzania.
Hapa Tanzania changamoto ya idadi ya watu, haitazamwi kwa umakini unaostahili. Pamoja na kuwa kuna baadhi ya watu wanazungumza suala hilo, inaonekana kuwa lipo vinywani tu. Bado baadhi yetu tunaamua tu kuzaa kwa kuwa tumefikisha umri fulani, sio kwa kuwa kweli tunahitaji kuwa na watoto, uwezo wa kukabiliana na majukumu ya kuwa na mtoto au sisi wenyewe kuwa wazazi, au tunaiga mkumbo na kuchagua kuwa na idadi ya watoto tunaopenda kuwa nao bila kuzingatia kama tuna uwezo wa kuwatunza na kuwawezesha waishi maisha bora, na baadhi tunachukulia fahari na kuona ni jambo la kawaida kuwa na watoto nje ya ndoa, kuwatelekeza na kuwafanya wengine wawe watoto wa mitaani. Ni kawaida kuona mtu ana watoto watano, lakini kimsingi hana hata uwezo wa kiuchumi wa kumudu kumtunza mtoto mmoja, lakini ukiuliza ni kwanini ana watoto wengi, huwezi kupata jibu la maana, zaidi ya kusema Mungu atawaangalia.
Sera ya mtoto mmoja ya China ina dosari zake, na wachina wenyewe wanajua dosari hizo, na kwa sasa kuna mjadala unaoendelea kuhusu kuifanyia mabadiliko sera hiyo ili iendane na mazingira ya sasa. Siwezi kusema kuwa sera hiyo inafaa kwa Tanzania au la, kwa kuwa kuna mambo mengi yanaoendana na sera hiyo ambayo yako kinyume kabisa na maadili, utamaduni na mazingira ya Tanzania. Lakini pia kuna mambo mengi yaliyomo kwenye sera hiyo, ikiwa ni pamoja na mantiki ya sera yenyewe, yanayoweza kuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania na watanzania.
Ni bora kuwepo na sera ya maana inayotekelezwa na kulalamikwa, kuliko kutokuwa kabisa na sera au kuwa sera midomoni na kwenye makaratasi tu, na kuacha ongezeko la idadi ya watu liendelee kuwa bomu linalokaribia kulipuka.
Tunachotakiwa kukumbuka ni kuwa, sera inayohusu idadi ya watu ni sera muhimu kwa taifa inayopaswa kupangwa kwa uangalifu sana tangu mwanzo, kwani athari au manufaa yake hayaonekani mara moja, lakini hakika sera ya namna hiyo inaweza kuwa na manufaa kwa taifa pamoja na mwananchi mmoja mmoja baada ya miaka 10 hadi 20, wakati watu wa kizazi kimoja watakapokuwa wamekua, kuingia kwenye soko la ajira na kutaka maisha bora.
Sera ya uzazi wa mpango ya China ilianza kutekelezwa miaka 70 karne iliyopita, ili kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu. Kimsingi sera hii inawataka kila wanandoa wachina wawe na mtoto mmoja. Nimeamua kutumia neno “kimsingi” kwa kuwa si wanandoa wote wanaotakiwa au wanaolazimishwa kuwa na mtoto mmoja kama baadhi ya watu wanavyoambiwa na kuamini.
Sera hii kwanza inawalenga watu wa kabila kubwa zaidi la China, yaani wa-Han, ambao wanachukua zaidi ya 95 ya idadi ya watu wote wa China. Watu wa makabila mengine ambayo nchini China yanaitwa makabila madogo madogo wanaweza kutekeleza sera hiyo kwa hiari, na baadhi yao hata wanapewa ruzuku kutokana na kufuata sera hiyo kwa hiari. Hata hao wa-han si wote wanaotakiwa kutekeleza sera hiyo kama sera inavyoelezwa, kuna wakati baadhi hawabanwi sana na sera hiyo.
Kwa mfano, wa-han wachina wanaoishi vijijini wanaotegemea shughuli za kilimo, sera hii haiwabani sana kwa kuwa wanahitaji nguvu zaidi, kwa hiyo wanaweza kuwa na mtoto zaidi ya mmoja. Wa-han wa mijini ambao wote ni mtoto pekee kwenye familia zao, wakioana wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Wa-han wanaobanwa na sera hii wakienda kinyume wanatozwa faini. Kwa hiyo ukiangalia vizuri unaweza kuona kuwa, kwa wachina wa kabila la wa-han sera hii ni kama sheria, lakini kwa wachina wa makabila mengine ni sera ambayo utekelezaji wake ni hiari.
Hebu kwanza tutupie macho hali nchini China katika miaka ya 1970 wakati ilipoamua kutekeleza sera ya uzazi wa mpango. Jamhuri ya watu wa China ilianzishwa mwaka 1949 baada ya mapigano na vita vilivyodumu kwa karibu miaka 100 nchini China. Mwaka 1949 idadi ya wachina ilikuwa milioni 550, na kwa wastani watu waliokuwa wanaishi miaka 35. Lakini hadi kufikia mwaka 1980, idadi ya watu wa China iliongezeka na kufikia bilioni 1 na umri wa wastani wa maisha ya mchina pia uliongezeka na kufikia miaka 68. Kutokana na makadirio yaliyofanyika mwaka 1980, idadi ya watu wa China ingeweza kufikia bilioni 1.4 hadi ifikapo mwaka 2000.
Ukiangalia sababu nyingi zilizowafanya wachina waanze kutekeleza sera hii, unaweza kuona kuwa kuna mazingira mengi yanayofanana na hali ya sasa ya Tanzania. Idadi kubwa ya watu ni shinikizo kubwa sana kwa maliasili na raslimali za jamii kama vile ardhi, maji, chakula, shule, hospitali na miundo mbinu mingine. Mwanzoni mwa miaka ya sabini changamoto hizo zilikuwa ni mzigo mkubwa sana kwa wachina, na ni changamoto hizo hizo ambazo kwa sasa sisi watanzania tunalalamika nazo kila kukicha. Lakini changamoto hizo hazipo kwa Tanzania peke yake, bali pia zipo katika maeneo mengine duniani, ambako maliasili zinaendelea kupungua.
Nchini China watu walijua kuwa kama wakiendelea kuzaliana kwa wingi, basi ingekuwa ndoto au ingechukua muda mrefu kuwa na ongezeko la uchumi, na hata kama kungekuwa na ongezeko lolote la uchumi, ongezeko hilo lingefutwa na ongezeko la idadi ya watu. Kwa sasa hapa Tanzania tunasema kasi ya uchumi wa nchi yetu inaongezeka kwa asilimia zaidi ya 5 na 6 hivi. Hii kwa kweli ni habari nzuri, lakini ongezeko hilo halionekani kwenye maisha ya mtanzania wa kawaida, inawezekana kuwa ongezeko hilo linafutwa na ongezeko la idadi ya watu.
Hata tukiangalia familia moja moja, ni wazi kuwa ukiwa na watoto wengi kuliko uwezo wako wa kuwamudu, kwanza kama mzazi utatumia muda mwingi kujaribu kuwatunza watoto wako, na pili unaweza kukosa muda wa kutosha kutumia akili zako na nguvu zako kufanya mambo mengine yanayoweza kukunufaisha wewe na kulinufaisha taifa.
Mbali na maelezo yanayotolewa na serikali ya China kuhusiana na manufaa ya kiuchumi yanayotokana na utekelezaji wa sera hii, ukiwauliza wachina wa kawaida hasa wa mijini, wanakwambia kuwa hata kama isingekuwa sera ya serikali, wengi wao wanalazimika kutekeleza sera hiyo kutokana na mazingira ya sasa ya kiuchumi. Si rahisi kumudu kununua nyumba ya kuwatunza watoto watano, si rahisi kununua chakula cha kuwalisha watoto wengi namna hiyo, na zaidi ni vigumu sana kumudu gharama za elimu, matibabu na huduma nyingine kwa ajili ya watoto. Kwa ufupi ni kwamba, kuwa na idadi kubwa ya watoto, kwa mazingira ya nchi kama China, hasa mijini, ni kujiletea matatizo makubwa.
Hata hivyo sera yoyote lazima iendane na hali halisi. Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na ongezeko la uchumi na kuinuka kwa kiwango cha maisha, wachina hasa wakazi wa mijini katika maeneo yaliyoendelea kiuchumi, wanandoa vijana wanaonesha nia ya kuahirisha umri wa kuzaa mtoto, na baadhi yao kuamua kutooana au kutozaa.
Kwa upande mwingine wazee wanaishi kwa muda mrefu zaidi, hali ambayo inafanya kuwe na wazee wengi katika jamii ya China. Ndiyo maana pamoja na kuendelea na juhudi za kudhibiti ongezeko la kasi la idadi ya watu, serikali ya China imeanza kufikiria na kuchukua hatua ya kurekebisha sera yake ya uzazi wa mpango. Hatua moja ni kwamba, wanandoa ambao wao ni mtoto pekee kwenye familia, wanaruhusiwa kuwa na watoto wawili. Na serikali pia ilichagua baadhi ya maeneo kufanya jaribio la watoto wawili, lakini watu wengi waishio maeneo hayo hawapendi kuzaa mtoto zaidi ya mmoja, tofauti na ilivyodhaniwa. Kuna wachina wengi tu ambao wanaamua kuoana na kutozaa, labda kutokana na utamaduni wa sisi waafrika jambo hili halifikiriki.
Pamoja na kuwa sera hii imeshambuliwa na jumuiya za haki za binadamu duniani na taasisi za kidini, hasa kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya utoaji mimba hasa inapojulikana kuwa ni mtoto wa kike, na kutokana na kinachotajwa kuwa ni kuzuia uhuru wa mtu kuamua idadi ya watoto anaotaka, lakini tukiangalia lengo la kimsingi la uwepo wa sera hii—kulinganisha matokeo ya uzalishaji wa mtu mmoja moja na thamani ya uzalishaji wa mali na maendeleo ya uchumi na jamii kwa ujumla, tunaweza kusema sera hii kimsingi imekuwa na manufaa kwa mtu mmoja mmoja, familia na nchi kwa ujumla.
Inakadiriwa kuwa sera hii imepunguza ongezeko la idadi ya watu kwa watu milioni 400, maana yake ni kuwa maliasili na rasilimali ambazo zingetumika kwa ajili ya watu hao milioni 400, sasa zinatumika kuboresha maisha ya watu waliopo sasa. Afya ya kina mama wanaojifungua na huduma wanazopata wakati wa kujifungua vyote vimeboreshwa, na kutokana na kutokuwa wajawazito mara kwa mara, kina mama wanashiriki zaidi kwenye shughuli za uchumi, na hata watoto wanakuwa na afya zaidi, mazingira mazuri zaidi ya elimu na hata kuwa na mustakbali mzuri zaidi.
Tanzania tumewahi kuwa na kampeni kubwa iliyokuwa inatoa mafunzo mazuri sana kuhusu afya ya uzazi na hata manufaa yake kwa mlengwa, ikishirikisha taasisi zisizo za kiserikali. Pamoja umuhimu wake, kampeni hiyo ilikosolewa na baadhi ya taasisi za kidini, lakini ilionesha mwelekeo mzuri. Sijui kwa sasa Chama Cha Uzazi wa Mpango na Malezi bora UMATI kilichokuwa kinahimiza kampeni hiyo kinachukuliwa vipi, kina mwelekeo gani na kina uwezo gani wa kuhimiza upangaji wa sera za taifa kwenye mambo ya uzazi na kusimamia utekelezaji wake. Kama Chama hiki kikipewa msukomo zaidi wa kufanya kazi na kuwafikia watanzania wengi, kuna uwezekano kuwa chama hiki kitakuwa ni jibu la tatizo la ongezeko la idadi ya watu Tanzania. Kwa kuwa chama hiki kinajua vizuri mazingira ya watanzania kiuchumi, kidini na hata mienendo ya uzazi ya watanzania.
Hapa Tanzania changamoto ya idadi ya watu, haitazamwi kwa umakini unaostahili. Pamoja na kuwa kuna baadhi ya watu wanazungumza suala hilo, inaonekana kuwa lipo vinywani tu. Bado baadhi yetu tunaamua tu kuzaa kwa kuwa tumefikisha umri fulani, sio kwa kuwa kweli tunahitaji kuwa na watoto, uwezo wa kukabiliana na majukumu ya kuwa na mtoto au sisi wenyewe kuwa wazazi, au tunaiga mkumbo na kuchagua kuwa na idadi ya watoto tunaopenda kuwa nao bila kuzingatia kama tuna uwezo wa kuwatunza na kuwawezesha waishi maisha bora, na baadhi tunachukulia fahari na kuona ni jambo la kawaida kuwa na watoto nje ya ndoa, kuwatelekeza na kuwafanya wengine wawe watoto wa mitaani. Ni kawaida kuona mtu ana watoto watano, lakini kimsingi hana hata uwezo wa kiuchumi wa kumudu kumtunza mtoto mmoja, lakini ukiuliza ni kwanini ana watoto wengi, huwezi kupata jibu la maana, zaidi ya kusema Mungu atawaangalia.
Sera ya mtoto mmoja ya China ina dosari zake, na wachina wenyewe wanajua dosari hizo, na kwa sasa kuna mjadala unaoendelea kuhusu kuifanyia mabadiliko sera hiyo ili iendane na mazingira ya sasa. Siwezi kusema kuwa sera hiyo inafaa kwa Tanzania au la, kwa kuwa kuna mambo mengi yanaoendana na sera hiyo ambayo yako kinyume kabisa na maadili, utamaduni na mazingira ya Tanzania. Lakini pia kuna mambo mengi yaliyomo kwenye sera hiyo, ikiwa ni pamoja na mantiki ya sera yenyewe, yanayoweza kuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania na watanzania.
Ni bora kuwepo na sera ya maana inayotekelezwa na kulalamikwa, kuliko kutokuwa kabisa na sera au kuwa sera midomoni na kwenye makaratasi tu, na kuacha ongezeko la idadi ya watu liendelee kuwa bomu linalokaribia kulipuka.
Tunachotakiwa kukumbuka ni kuwa, sera inayohusu idadi ya watu ni sera muhimu kwa taifa inayopaswa kupangwa kwa uangalifu sana tangu mwanzo, kwani athari au manufaa yake hayaonekani mara moja, lakini hakika sera ya namna hiyo inaweza kuwa na manufaa kwa taifa pamoja na mwananchi mmoja mmoja baada ya miaka 10 hadi 20, wakati watu wa kizazi kimoja watakapokuwa wamekua, kuingia kwenye soko la ajira na kutaka maisha bora.
Post a Comment