Mujahidina wa Al-Shabab jana usiku walifanya mashambulio makubwa
katika uwanja wa Ndege wa mji wa Kismaayo ambayo ni kambi kubwa kwa
Wanajeshi wavamizi wa Misalaba kutoka Kenya katika mkoa wa Jubba.
Kikosi
hicho kilichofanya mashambulio kwenye kambi hiyo walirusha mizinga
kadhaa na baadae walianza kuzishambulia kwa risasi za rashasha dhidi ya
kambi hiyo ya Wanajeshi wa Kenya na inaarifiwa kuwa kulitokea mapambano
yaliodumu masaa kadhaa katika eneo hilo.
Maofisa
wa Mujahidina katika Mkoa wa Jubba tulipo wauliza kuhusu mapambano hayo
wametuthibitishia kuwa vikosi vyao walifanya mashambulio kwenye Kambi
ya Wanajeshi wa Kenya yalioko katika Uwanja wa Ndege wa mji wa Kismaayo
Aidha mujahidina baada ya kumaliza lengo lao la kuwapa maumivu maadui
waliondoka na kurudi kwenye maeneo yao.
Wanajeshi
wa Kenya walioko katika mkoa wa Jubba wamekutana na hali mbaya ikiwa ni
pamoja na kukatishwa mawasiliano ya wao kwa wao kwa njia ya Barabara,na
Wanajeshi wao walioko katika viwanja vya mapambano kushindwa kupata
shehena au msaada wa silaha na vivaa vya kijeshi kutoka kwa wenzao,na
kila siku hukutana na mapigano.
Post a Comment