0



Waziri wa ulinzi nchini Afrika kusini ametangaza kuwa jeshi litatumwa wakati ghasia dhidi ya wageni zikiwa zimesababisha vifo vya watu Saba.
Nasiviwe Mapisa-Ngqakula anasema kuwa ombi la kutumwa kwa wanajeshi liliamuliwa baada ya polisi kuomba msaada.
Lakini hakusema ni wanajeshi wangapi watatumwa mitaani. Jeshi litatumwa kwenda maeneo yanayoshuhudia ghasia nyingi ikiwemo mikoa ya Kwa Zulu Natal na Guateng.
Wakati wa ghasia kama hizo mwaka 2008 jumla ya watu 63 waliuawa. Serilali ya Afrika Kusini pia imetangaza kuwa zaidi ya watu 900 wamerudi kwa hiari kwenda nchi zao.

Post a Comment

 
Top