0





Wapiganaji wa kundi la Islamic State wameweka kanda ya video katika mtandao ambayo inamuonyesha mvulana mdogo akimpiga risasi na kumuua mfungwa mmoja mwenye asili ya kiyahudi na kiarabu.
Mtu huyo anayejulikana kama Mohammed said Ismail Musallam anatuhumiwa na kundi la IS kwa kulifanyia kazi kundi la upelelezi la Israel Mossad.
Kijana huyo mwenye miaka 19 aliondoka nyumbani kwao mashariki mwa Jerusalem kwenda Uturuki mwaka uliopita ili kujiunga na kundi la IS nchini Syria.
Maafisa wa Israel na familia ya Mussallam zimekana kwamba alikuwa mpelelezi wa Israel.
Kanda hiyo ya Video haijathibitishwa na maafisa wa Israel wanasema kuwa hawawezi kuthibitisha chimbuko lake.
Familia ya Mussallam imesema kuwa alielekea nchini Uturuki miezi minne iliopita bila kuwaarifu.

Post a Comment

 
Top