Shoo hiyo iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu imepangwa kufanyika hapo October 3, katika uwanja wa Namfua.
Wasanii watakaotumbuiza ni pamoja na Mwana FA, Nikki II, Makomando, Stamina, Ney, Young Killa, Linah, Recho, Mr. Blue, Dully Sykes, Mo Music na Baraka Da Prince.
Mwana FA atatumbiza kwa mara ya kwanza katika shoo za tamasha la hilo mwaka huu mjini humo.
“Nimefarijika kuwa mmoja wa wasanii watakaotumbuiza mjini Singida na ningependa kuwashauri mashabiki wangu waje kwa wingi kunishuhudia jukwaani nikifanya mambo wakati wa shoo,” alisema.
Kabla ya shoo hiyo, kutakuwa na shughuli nyingine mbalimbali kama shindano la Serengeti Super Nyota Diva ambalo mshindi atajinyakulia tiketi kwenda kushuhudia shoo ya mwisho ya tamasha hilo litakayofanyika hapo Oktoba 18, 2014 jijini Dar es Salaam.
Post a Comment