Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza (kulia) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akizindua ushirikiano wa kampuni yake na Benki ya Afrika (BOA) Tanzania unaowawezesha mawakala wa M-pesa na wasambazaji wa huduma za Vodacom kupata miko nafuu na bila dhamana kuinuua biashara zao. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya BOA, Ammish Owusu – Amoah.Hafal hiyo imefanyika Makao Mkauu ya Vodacom, Dar es salaam
Chini ya mpango huu mawakala wa Vodacom wataweza kuchukua mkopo unaofikia mara 6 ya kamisheni wanayokuwa wamepata katika kipindi cha miezi 6 kabla ya kuomba mkopo. Wataweza kukopa kuanzia kiasi cha shilingi milioni 10 na kiasi cha juu ya kukopa ni shilingi milioni 75 .Mkopo huu ambao ni mkombozi kwa mawakala hao una riba ya asilimia 1.7 kwa mwezi na unatakiwa kulipwa ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Afrika (BOA) Tanzania Ammish Owusu – Amoah (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza wakipongezana mara baada ya kutangaza rasmi ushirikiano unaowawezesha mawakala wa M-pesa na wasambazaji wa huduma za Vodacoyam kupata mikopo nafuu na bila dhamana kutoka BOA kwa lengo la kuinuua biashara zao. Mikopo hiyo ni kati ya Sh 10 Milioni na 75 Milioni
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza,amesema kuwa mpango huu umeanzishwa kwa ajili ya kuwawezesha makala waliopewa jukumu kusambaza nchi nzima bidhaa za Vodacom ikiwemo vocha za kununua muda wa maongezi kuwa na mzunguko mzuri wa pesa utakaowawezesha kutoa huduma bora kwa wateja.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Afrika (BOA), Ammish Owusu – Amoah(kushoto)akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)kuhusiana na kuingia ubia na Vodacom Tanzania ambao utawawezesha mawakala wa kuuza na kusambaza bidhaa za kampuni hiyo kupata mikopo ya masharti nafuu na bila amana ili kuwawezesha kutoa huduma bora kwa wateja wao,kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Rene Meza
“Mpango huu utawawezesha mawakala wetu kuimarika kibiashara wakati huohuo kutoa huduma bora kwa wateja wetu na kiwango chao cha mauzo kitaongezeka.Kwetu Vodacom mpango huu ni wa muhimu sana na makala wa kuuza na kusambaza bidhaa zetu ambao watachangamkia fursa hii ambayo itawasaidia kufanya biashara kwa kujiamini na
kuhakikisha wateja wetu ambao kila kukicha wanaongezeka mara dufu wanapata huduma za kuridhisha popote walipo nchini,”alisema Meza.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Afrika (BOA)-Tanzania na wa Vodacom Tanzania wakifuatilia mkutano wa waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa ushirikiano kati ya BOA benki na Vodacom Tanzania
Kwa upande wake,Afisa mtendaji wa Benki ya BOA, Ammish Owusu – Amoah, amesema ushirikiano huu na Vodacom umefungua ukurasa mpya kwa benki,wateja wake na kwa wanajamii ya Tanzania kwa ujumla, kwa kuwa wanaelewa kiu ya wajasiriamali wa Tanzania wanavyohangaika kutafuta mikopo kwa ajili ya kukuza na kuboresha biashara
zao.
“Kama benki ili kufanikisha huduma hii ya kutoa mikopo tumeanzisha kitengo maalumu cha kusimamia huduma hii ya kutoa mikopo kwa wajasiriamali bila urasimu katika matawi yetu yote nchini pia benki itahudumia wateja wa M-pesa,”alisema Ammish. Alisema mpango huu ambao umezinduliwa leo unawawezesha wauzaji na wasambazaji wa
bidhaa za Vodacom kupatiwa mtaji wa kufanya biashara zao wanapotaka kukununua bidhaa nyingi zaidi ya mtaji walionao.Mkopo unaanzia shilingi milioni 10 mpaka milioni 75 kwa awamu ya kwanza na kwa wateja watakaotimiza vizuri taratibu na masharti ya mkopo wanaweza kufikiriwa kupatiwa mkopo mkubwa zaidi ya shilingi milioni 75.
Aliongeza kuwa huduma hii inawalenga wauzaji na wasambazaji wakubwa wa bidhaa za Vodacom zaidi ya 100 ambao wataweza kununua bidhaa kupitia matawi ya BOA-Tanzania na pesa zitaingizwa katika akaunti ya Vodacom iliyopo kwenye benki hiyo na ana imani huduma hii itawarahisishia kufanya biashara zao kwa kupata bidhaa wanazohitaji
haraka kutoka Vodacom.
Vodacom imekuwa ikibuni huduma mbalimbali za kuwarahishia wananchi maisha.Moja ya huduma ni M-pesa ambayo tangu ianzishwe hapa nchini imepokelewa vizuri na wananchi ikiwa inarahisisha maisha wakati huohuo ikiwa imetoa ajira kwa wananchi wengi.Mpaka sasa mtandao wa M-pesa una mawakala wapatao zaidi ya 70,000.
Mawakala watakaohitaji kupata mkopo huu watapaswa kutembelea matawi ya benki ya BOA- Tanzania ambayo yako katika mikoa ya Dar es Salaam ambako ina matawi 11 na matawi mengine yapo katika mikoa
ya,Arusha,Shinyanga-Kahama,Kilimanjaro,Mbeya,Morogoro,Mtwara na Mwanza.
Benki ya BOA Tanzania iko chini BOA Afrika,kwa hivi sasa inaendesha shughuli zake za kibenki katika nchi 17 za Afrika na nchi moja ya Ulaya ambazo ni : Benin, Burkina Faso, Burundi, Djibouti, Ethiopia, Togo, DRC, France, Ghana, Ivory Coast, Kenya, Madagascar, Mali, Niger, Senegal, Tanzania and Uganda.
Post a Comment