Mazungumzo ya amani yafanyika kumaliza mapigano Gaza
Kiongozi wa ujumbe wa
Wapalestina walioko katika mazungumzo ya amani huko Cairo amesema
usitishaji mapigano huko Gaza unaweza kuendelea kwa siku tano zaidi.
Maamuzi hayo yamefikiwa ikiwa imesalia karibia
saa moja tu kuisha kwa muda wa saa 72 wa usitishaji mapigano kuisha.
Afisa wa Palestina Azzam al-Ahmad amesema kumekuwa na maendeleo mazuri
wakati wa mazungumzo ya amani yanayosimamiwa na Misri.Lakini hakuna taarifa yoyote kutoka upande wa Israel zaidi ya kuwa kulikuwa na shambulizi la roketi kutoka Gaza na hivyo kusababisha wapiganaji wa Israel kulipiza kwa kutumia mashambulizi manne ya anga.
Hata hivyo wapiganaji wa Kipalestina wamekanusha kuhusika na mashambulizi ya awali.
Post a Comment