Unapozungumzia wanawake wanaofanya vizuri kwenye muziki duniani,
lazima Rihanna atakuwa kwenye orodha hiyo kutokana na uwezo wake mkubwa
katika fani hiyo yenye mashabiki wengi kila kona ya ulimwengu.
Licha ya uwezo wake mkubwa alionao katika uimbaji ni miongoni mwa wanamuziki wa kike, wenye muonekano na haiba ya aina yake.
Uzuri wa sura na umbo lake unamfanya kuwa mwanamke
ambaye anavutia kutazamwa na watu wa jinsia zote, hasa wembamba na
urefu wake mithili ya twiga.
Kama walivyo warembo wake, mwanamuziki huyu
hutumia umbile lake hilo kuvaa nguo za mitindo ya kila aina ambayo mingi
kati ya hiyo humfanya kuvutia zaidi.
Mvuto huo ulimfanya kupewa sifa ya ubalozi wa
mitindo na kuwa miongoni mwa wasanii ambao wanasifika kwa kwenda na
wakati hasa katika sekta nzima ya mitindo.
Huenda sifa hiyo ndiyo imemfanya hivi karibuni
kuzua gumzo katika maeneo mbalimbali kutokana na aina ya nguo ambazo
mwanadada huyu hutoka nazo hadharani huku akitambua fika kuwa zinaacha
wazi sehemu kubwa ya mwili wake.
Zaidi ya mara tatu Rihhana ameonekana akiwa katika
mavazi ya ajabu, ambayo mwisho wa siku hupelekea kuibuka kwa
majadiliano katika mitandao ya kijamii.
Kana kwamba hiyo haitoshi ilifika wakati mtandao
wa Instagram ulilazimika kuifunga akaunti ya mwanamuziki huyo kutokana
na kuweka picha ambazo zinamuonyesha akiwa na mavazi yasiyostahili.
Ingawa kujadiliwa kwa mtindo huu kunachangia
kuzidi kumuongezea umaarufu nyota huyu, lakini kwa upande mwingine
amekuwa akiwachukiza baadhi ya mashabiki wake ambao wanaonekana wazi
kukerwa na mwenendo huo.
Pamoja na hitilafu hiyo katika mavazi Rihanna bado ni miongoni mwa wasichana wanaofanya vizuri kwenye ‘game’ mpaka hivi sasa.
Nyota ya mwanadada huyu asiyeishiwa na vituko
ilianza kung’ara mwaka 2005, alipotoa nyimbo kadhaa zikiwemo Music on
the Sun, A girl like me.
Uwezo wa hali ya juu wa nyota huyu ulionekana
mwaka 2006 alipoachia wimbo wa Pon de Replay ambao ulionekana kubamba
katika chati cha muziki ulimwenguni kote.
Diamonds, Disturbia, Te Amo, Rehab, Unfaithfully, Only girl ni
miongoni mwa kazi zake ambazo zimefanya vizuri na kumwezesha kutunikiwa
tuzo tatu za Grammy mpaka sasa ukiachilia mbali tuzo nyingine kadhaa
ambazo anazo mwanadada huyu.
Rihanna kwa sasa yuko kwenye maandalizi ya kuachia
albamu yake ya nane baada ya saba za awali kufanya vizuri kwenye mauzo,
kiasi cha kuweka rekodi ya kuwa mwanamuziki anayefanya vizuri sokoni.
Miongoni mwa albamu ambazo zilishatoka ni pamoja
na Music on the Sun, A girl like me, Good girl gone bad, Rated R, Loud,
Talk that Talk na Unapologetic.
Imeandaliwa na Elizabeth Edward kwa msaada wa mashirika ya habari
Post a Comment