Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Tanzania imesema kuwa hadi kufikia leo Septemba 23, 2013 ni Mtanzania mmoja tu aliyetambulika kwa jina la Bwana Vedastus Nsanzugwanko mwenye cheo cha Umeneja katika kitengo cha Ulinzi wa Watoto, cha Shirika la Umoja wa Mataifa la Hazina ya Kuhudumia Watoto (Child Protection, UNICEF) ambaye taarifa zake ziliifikia Ofisi ya Balozi kuwa amejeruhiwa kwa risasai na milipuko ya maguruneti kwenye miguu yake yote miwili.

Taarifa hiyo inasema kuwa kwa sasa hali Bwana Vedastus inaendelea vizuri akiwa anapatiwa matibabu alikolazwa katika hospitali ya Aga Khan ya jijini Nairobi, Kenya.