0

Maeneo ya Mwabepande yanavyoendelea kuchakaa kama yanavyoo onekana. Picha na Kalunde Jamal.  

Dar es Salaam. Anaendelea kusimulia kuwa baada ya kuapata somo hilo mwanae akasema wasome dua kila mmoja ya kwake wakimshirikisha na baba yake, kwa kuwa hali ilikuwa ni ya hatari na maji ni mengi na yalikuwa yanazidi kujaa. “Tukasoma dua na kila baba yake alipokuwa akituhimiza kuondoka, kijana alisisitiza tuendelee kusoma akiamini hata kama tukifa kila mmoja afe akiwa salama,” anasema.
Zainabu anaongeza kuwa baada ya dua walijitosa majini na kufanya kama alivyoambiwa kwa bahati nzuri walifika salama nchi kavu, lakini kijana wake alimzia mara kadhaa.
“Cha kushangaza baada ya kufika nchi kavu kijana wangu alianza kuzimia mara kadhaa, kila akizinduka anazimia tena, lakini akapatiwa huduma ya kwanza na baada ya kurudi kwenye hali ya kawaida akasema haamini kama ameniokoa na hata alipokuwa akiniokoa hakuwa yeye bali ni bua, kwani alikuwa amekata tamaa ya maisha yao tena,” anasema Zainabu huku akisema kisa hicho ndiyo kinamfanya avumilie lolote linalotokea katika jangwa hilo.
Anasema kuwa kamwe hawezi kurudi kule tena na kuiomba Serikali kuwafikiria na kulifanyia kazi suala lao mapema kama alivyoagiza Rais.
Wakazi wengine wanaizungumziaje hali hiyo
Hashimu Saidi ni moja ya wakazi waliopata hifadhi katika eneo hili anasema kuwa alipopata matatizo na kuhamia katika eneo hilo, alikuwa na familia yake ambayo ilikuwa ni mkewe na wanawe wawili, lakini amelazimika kumrudisha mkewe kwao Lindi kutokna na hali kuwa ngumu.
Anasema wakati wanafika eneo hilo mwaka jana kulikuwa na mvua wakapewa mahema ambayo waliambiwa yanadumu kwa miezi sita hadi nane, lakini sasa ni zaidi ya mwaka bado wanaishi katika mahema hayo ambayo kwa sasa hayafai tena.
“Kipindi tunakuja huku kulikuwa na mvua za msimu huu zimenyesha, tena yameraruka na limekuwa siyo eneo salama la kuishi kwa kuwa hali ni mbaya upepo kama unavyoona,” anasema Saidi na kuongeza kuwa:
“Nikiona kipande cha bati hata kama ni mbali vipi naokota, nikiona boksi naokota kila ambacho naamini kitanisaidia kuziba hema hili naokota, ndiyo maana nimemudu kuwa hapa hadi leo lakini hali ni mbaya sana,” analalamika Saidi.
Aidha, Saidi anasema kuwa kibaya zaidi waliahidiwa kupata mifuko 100 ya sementi kutoka kwa Rais na mabati 30, ambayo ilikuwa ni ahadi ya mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Center ambayo aliitoa mbele ya Rais alipowatembelea, lakini cha kushangaza hadi sasa hakuna kinachoendelea na hawajui wamuulize nani.
Anaendelea kulalamika kuwa hata viongozi waliokuwa wakifika eneo hilo kwa ajili ya kuwapa taarifa hizi na zile sawa hawafiki tena, licha ya Rais kutoa angalizo wabadilishiwe mahema na Chama cha Msalaba Mwekundu hivyo nacho hadi sasa hakijafanyika.
Mwananchi ilimtafuta Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam , Said Meck Sadiki, amelitolea ufafanuzi suala la sarujiambalo Rais aliagiza wakazi hao wapewe, kwa kusema kuwa mchakato unaendelea lakini unafuata sheria za ununuzi wa Serikali na ndiyo maana unachukua muda mrefu kukamilika.
Alisema kuwa fedha za Serikali hazitoki kama njugu au pipi kama wanavyotaka wakazi wa maeneo hayo, bali zinahitaji mipangilio maalumu ikiwamo kufuata sheria na utaratibu uliowekwa.
Mkuu huyo pia alizungumzia uamuzi uliochukuliwa na wakazi wa eneo hilo kurudi katika maeneo yao ya awali, kwa madai kuwa mahema waliyopewa yamekwisha na hakuna utaratibu mwingine wa kupewa mapya, kuwa hakuna mpango wa kupewa mengine na hiyo ipo duniani kote kuwa msaada unakuwa ni kwa mara ya kwanza na wala siyo siku zote kama wanavyodhani wao.
“Ule ulikuwa ni msaada wa ghafla na kizuri zaidi na maeneo wamepewa kwa muda wote huu wameshindwa kujenga hata vibanda imara vya kuishi wanasubiri mahema mengine watayapata wapi hakuna mpango huo”alisema Sadiki.
Aidha Sadiki alitoa ufafanuzi kuhusu wakazi wa eneo hilo waliorudi mabondeni, kuwa shauri yao hakuna atakayewafunga kamba na yatakapotokea mafuriko wasitegemee kupata msaada tena, kwa kuwa wameamua wenyewe kwa makusudi kurudi sehemu ambayo si salama.
“Tuliwasaidia kwa kuwa hawakuwa na pa kwenda na hakukuwa na utaratibu wa kuwahamisha kule hapo kabla lakini sasa eneo lipo na kila mmoja amepewa la kwake, sasa kama yupo aliyerudi kwa hiyari yake akidhani anaikomoa Serikali shauri yake, hatuwezi kuwafunga kamba au kubembeleza warudi,” alisema Sadiki.

Post a Comment

 
Top