Katika maazimio yao wamekubaliana kufanya kampeni
za kuing’oa CCM madarakani kuanzia ngazi za vitongoji, vijiji, mitaa,
kata, majimbo hadi Taifa katika chaguzi mbalimbali endapo Serikali
itakataa kuunda tume huru ya kuchunguza sakata zima la Sheikh Ponda
kushambuliwa kwa risasi alipokuwa katika mkutano wa Waislamu mjini
Morogoro Agosti 18 mwaka huu.
Akizungumza katika mkutano ulioshirikisha Waislamu
kutoka Wilaya ya Kigoma, Mwenyekiti wa Shura ya Maimamu Mkoa wa Kigoma,
Sheikh Ibrahim Ramadhan alisema kamwe hawatakubaliana na taarifa yoyote
itakayotolewa na Polisi kwa sababu wamepoteza imani na jeshi hilo.
Pia alilaani kauli iliyotolewa na Kamanda wa
Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova kwamba polisi wapo
tayari kupambana na yeyote atakayeonekana kuandamana kutaka Ponda
aachiwe.
Alilaumu kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
aliyotoa bungeni kuwataka Polisi kupiga wananchi kwa kisingizio cha
kutotii sheria kuwa ndizo zinazosababisha viongozi wa dini kupigwa na
polisi mara kwa mara kwa kupata vipigo bila sababu za msingi.
Post a Comment