MKAZI wa kijiji cha Ndanga wilayani Kyela mkoani Mbeya, Edward
Mwakalebela (86), ambaye ni mganga wa tiba za jadi, anatuhumiwa kumbaka
mtoto mwenye umri wa miaka sita (jina tunalo). Akizungumza na MTANZANIA
jana, mama mzazi wa mtoto huyo, Sioni Ijuni, alisema tukio hilo
lilitokea juzi. Alisema mtoto huyo, alikuwa akilalamika maumivu ya tumbo
na ndipo mama yake aliamua kumpa huduma ya kwanza kwa kumkanda na maji
ya moto.
Alisema baada ya kumkanda, ghafla alianza kuona damu zikitoka sehemu za siri.
Alisema alipomhoji mtoto huyo, alimtaja babu huyo kuwa alimuingilia kimwili na kumfanyia kitendo hicho cha kinyama.
Mzee huyo, ambaye wanaishi jirani, alikuwa na mazoea ya kumtuma mtoto mara kwa mara kama vile mjukuu wake.
Kutokana
na hali hiyo, mama huyo aliamua kupeleka taarifa kwa mwenyekiti wa
kijiji, akiwa na mume wake, Kifoji Mwabusila, ambaye walitengana na
wanaishi mbalimbali.
Alisema walipofika kituo cha Polisi,
walipewa kibali kwa ajili ya kwenda kupatiwa matibabu katika hospitalini
ya wilaya ya Kyela na polisi kwenda kumkamata mtuhumiwa na kumtia
hatiani.
“Tulipokuwa kwa mwenyekiti wa kijiji, babu huyo alikiri
kutenda kosa hilo na aliomba msamaha akidai ni shetani tu alimpitia,
huku akiomba mambo hayo yamalizwe kimya kimya bila kwenda polisi, jambo
ambalo lilikuwa gumu kwetu kulikubali,” alisema.
Mwenyekiti wa
kijiji hicho, Dickson Mwakasinga, alikiri kuwepo kwa tukio hilo na kuwa
baada ya kuletewa taarifa, alifuata taratibu zote na kumkabidhi
mtuhumiwa huyo mikononi mwa polisi wilaya kwa hatua zaidi za kisheria.
Kwa
upande wake, mganga Tabu Mwakalundwa alikiri kumpokea mgonjwa huyo na
kudai kuwa mtoto huyo aliingiliwa na kuharibiwa vibaya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment