0




Sherehe zimefanyika eneo la Gallipoli nchini Uturuki kuadhimisha miaka mia moja tangu uvamizi wa kijeshi uliofanywa eno hilo na wanajeshi wa muungano wakati wa vita vya kwanza vya dunia.
Zaidi ya watu 100,00 waliuwa kwenye uvamizi huo ulioendeshwa dhidi ya ufalme wa Ottoman.
Wageni kutoka nchi zote zilizopigana walihudhuria sherehe hizo wakiwemo viongozi kutoka Uturuki , Australia na New Zealnd, ambazo zote zilipoteza watu wengi.
Sherehe pia zilifanyika mapema nchini New Zealand na pia mjini Sydney. Zaidi ya wanajeshi 10,000 wa Australia na New Zealand waliuawa kwenye vita hivyo vilivyofeli.

Post a Comment

 
Top