0
Askari akimburuza Muislaam bila huruma katika mauaji ya kihitoria ya Mwembechai Mosque Killings 1995 mjini Dar Es Salaam
Madhila baado yamendelea kwa jamii ya kiislaam nchini Tanzania baada ya Serikali kibaraka ya nchi hiyo kuja na mkakati na mbinu mpya wa kupambana na Uislaam wa kupinga watoto wa kiislaam kufundishwa masoma ya Dini yao.



Habari kutoka Kanda ya Ziwa Magharibi mwa Tanzania zinaeleza kuwa Maaskari wa kupambana kwa kile walichokiita Ugaidi walikivamia chuo cha kuhifadhisha Qur'an kilichopo Ilemela mjini Mwanza siku ya jumamosi uliopita.




Walioshuhudia wanasema Maaskari hao wakiwa na Silaha zao walikivamia chuo hicho na kuwatoa baadhi ya vijana waliokuwa na Umri wa miaka 15 hadi 17 na kusema kuwa hawajafikia umri wa kusomeshwa kuhifadhi Qur'an.



Machi,7 mwaka huu Serikali kibaraka ya nchi hiyo iliwafukuza watoto 17 waliokuwa wakisoma chuo cha kuhifadhisha Qur'an katika mji wa Moshi.



Mkuu wa Wilaya wa Moshi Novatus Makunga amesema kwa sasa chuo hicho imefungwa na watoto wote wameondolewa na kurjeshwa kwenda kusoma shule ambazo huharibu ubongo za watoto wa Kiislaam.



Abdulnasir Abdurahim ambae ni mwalimu wa chuo hicho amesema chuo inawafundisha watoto wa Kiislaam kuhifadhi Qur'an tukufu ambayo ni msingi wa Dini yao.



Kati ya Machi 25 na 27 mwaka huu Maaskari wa kupambana na Uislaam waliingia kwa nguvu misikiti ya Bilal uliopo mtaa wa kibaoni Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro na Masjid Othman uliopo Uzunguni na kuwakamata watoto zaidi ya 147 na kudai kuwa walikuwa wakifundishwa masomo yalio kinyume na sheria.



Mkuu wa Wilaya ya Hai Anthony Mataka,amethibitisha kuwepo uvamizi huo wa Maaskari dhidi ya Misikiti hizo na kuwalaumu waalimu wa wanaofundisha masomo ya Dini.



"tukio hiyo lipo na wanaohusika ni watu wanaotumia mwamvuli wa Dini fulani kufanya mambo yasiofaa katika jamii,kwahiyo naziomba Mamlaka husika ikiwemo Baraza kuu la Waislaam (Bakwata) kutambua Misikiti na shughuli zinazoendelea katika nyumba hizo za Ibada,Hili lazima walifanyie kazi kwa sababu hao vijana inasemekana wanafundishwa mazoezi makali ya kareti na judo katika nyumba hizo za ibada,” alisema Mtaka.


Mbinu huu mpya wa Serikali ya Tanzania ni sehemu ya mkakati vita dhidi Uislaam inayolenga kuangamiza jamii ya Kiislaam walio wengi katika nchi hiyo iliyopo katika Bara la Afrika Mashariki.

Post a Comment

 
Top