Mkanda
huo wa video uloweza kutizamwa kwa kiasi cha muda wa dakika 12 ulitoa
pia ujumbe kwa vijana wa Kiislaam Afrika Mashariki khususan nchini
Tanzania na kuwataka vijana wa kiislaam kuungana dhidi ya Adui wao.
"Ndugu
zangu waislaam huu ni ujumbe kwa vijana wa Kiislaam wa Afrika Mashariki
khususan nchi ya Tanzania,sisi ni vijana wenzenu tupo Mkoa wa Tanga
tuliacha makazi yetu kwajili ya Allah (Subhanahu wata'alaa) na kuikufuru
Utawala unaoendeshwa kinyume na Sheria za Allah" alisema Mujahidi
aliyeonekana kwenye video hiyo.
Alionekana
mwenye kuwa na hasira huko akinyanyua Bunduki yake ya AK47 alioubeba na
kuinyanyua juu na kutamka Allahu Akbar yeye na mwenzake aliyebeba
Bunduki na Upanga kwenye mkono wake wa kulia wote kwa pamoja wakitamka
Allahu Akbar,Allahu Akbar.
"Sisi
ni kufru bitwaghuti,wallaahi hii ni ujumbe tunawaapa Makafiri na
kuwatangazia ndugu zetu waislaam kuwa njooni tuungane wakati
umefika...Allahu Akbar,Allahu Akbar".
Amesema
wao wako kwajili ya Allah na wameuza nafsi yao na wala hawaogopi huko
wakithibitisha kufanya mashambulio kadhaa kwenye maeneo mbalimbali na
kuionya Serikali ya Jakaya Kikwete.
Taarifa
nyingine ya kuwepo kwa mkanda mwingine wa video pia ilisambaa kwenye
vyombo vya habari na kusababisha khofu,mkanda huo wa pili unamwonyesha
mwanume aliyejitambulisha kwa jina la Abuu Kais Bin Abdallah ameionya
Serikali ya Tanzania na kuwa mashambulio makubwa yanakuja.
Abuu
Kais anathibitisha kuwa wao ndio waliotekeleza mashambulio yaliofanyika
vituo mbalimbali vya Polisi na kuawaua Maaskari kadhaa huko akitaja
kituo cha Polisi cha Ushirombo mkoani Geita na kile cha Ikwiriri na
kuongeza kuwa hakuna Mujahid aliyekamatwa.
TIZAMA PICHA ZA MUJAHIDINA WA TANZANIA HAPA CHINI
Post a Comment