0
Habari kutoka nchini Syria zinaeleza kuwa Wapiganaji wa Kiislaam pamoja na makundi ya wapinzani wamefanya mashambulio katika vituo vya jeshi la utawala wa Asad yalioko katika mkoa wa Idlib.



Makundi ya wapiganaji wa upinzani pamoja Makundi ya wapiganaji wa Kiislaam ikiwemo Jabhat Al Nusra yametangaza kuwa yalifanya uvamizi ya kuikomboa mji muhimu wa Kistratiji ya Jasru Shuqur iliyo upande wa Kaskazini mwa Syria na ni mji wa Pakee ambao umabakia kuishikilia Nidhamu ya Bashar Al Asad katika mkoa wa Idlib.



Duru ziliarifu kuwa wapiganaji wa Kiislaam wameuteka Vizuizi vyote vya mji wa Jasru Shuqur upande wa Kaskazini.


Vikosi vya Mujahidina wa Jabhat Al Nurah wamewavuka kwa nguvu jeshi la Asad huko wakiwaua makumi ya Wanajeshi wa Nidhamu hiyo ya Kishia,Waandishi wa habari wanasema wapiganaji wa Upinzani wanajaribu kuichukua Barabara zinazounganisha kati ya Idlib na Mkoa wa Pwani wa Ladiqiyah ambayo ni muhimu kwa nidhamu ya Kishia wa Asad.


TIZAMA VIDEO ILIYOANDALIWA NA AL-JAZEERA

Post a Comment

 
Top